Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

PANGA PANGUA UVCCM YAZIDI KUSHIKA KASI

Dar es Salaam. Hali imeendelea kuwa tete ndani ya Jumuiya ya Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UVCCM), huku jumuiya hiyo ikitengua uteuzi wa wakuu watatu wa idara zake ambao walikataliwa na Baraza Kuu la chombo hicho lililokutana hivi karibuni, Visiwani Zanzibar.
 

Wakati hayo yakiendelea kuna na taarifa kwamba kumekuwa na mwendelezo wa harakati za kuandaa mkakati wa kumwondoa madarakani mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Sadifa Juma Khamis na kwamba vikao vya kupanga mkakati huo vilianza mara tu baada ya mkutano wa Zanzibar.

Watendaji waliosimamishwa ni Wakuu wa Idara za Oganaizesheni, Tumaini Mwakasege, Fedha na Uchumi, Omary Suleiman na yule wa Idara ya Chipukizi na Uhamasishaji, Omary Justus.



Katibu Mkuu wa UVCCM, Sixtus Mapunda alilithibitishia gazeti hili kung’olewa kwa watendaji hao na kwamba kuendelea kwao na majukumu yao kutategemea iwapo watathibitishwa na Baraza Kuu la jumuiya hiyo linalokutana mjini Dodoma Oktoba mwaka huu.

“Sisi tuliomba hawa wathibitishwe kwenye kikao kijacho kwa kuwa kulitokea kidogo mkanganyiko wajumbe wakataka tujadili suala hili kwenye Baraza Kuu lililopita lakini kwa kuwa tulikuwa na ajenda moja tu ya kumthibitisha Katibu tukaomba suala hili lisogezwe mbele,” alisema Mapunda.

Mapunda alisema tayari watendaji hao walikuwa wameanza kazi lakini kutokana na baadhi ya kanuni kujikanganya, wameona ni vyema waache suala hilo mpaka kwenye mkutano ujao.

“Kuna kanuni inayotoa mamlaka kwa Kamati ya Utekelezaji na vilevile Baraza Kuu, kwa hiyo inabidi sasa tuweke kwanza mambo sawa kisha kwenye Baraza Kuu la Oktoba, hawa watathibishwa,” alisema.

Hata hivyo habari ambazo zimelifikia gazeti hili zinasema si rahisi kwa wakuu hao wa idara kurejea kwenye nafasi zao, kwani kitendo cha wajumbe kuwakataa katika kikao cha Zanzibar kinathibitisha kwamba hawana imani nao.

“Kama wajumbe wa Baraza Kuu wangekuwa wanawaamini, shinikizo lingekuwa ni kuwathibitisha, lakini sisi wajumbe ni kwamba hatuwataki. Inabidi Sadifa na kamati yake ya utekelezaji watuteulie watu wengine,” alisema mmoja wa viongozi wa UVCCM wa mikoa ambaye hakutaka kutajwa jina lake.

Suala la uteuzi wa wakuu wa idara za UVCCM pia ni mtihani wa kwanza kwa Katibu Mkuu mpya, Mapunda ambaye mara baada ya kuthibitishwa alionja chungu ya mgogoro katika taasisi ambayo yeye ni mtendaji mkuu wake, pale alipopingwa vikali na wajumbe, alipojaribu kumtetea Sadifa.

Katika mazingira hayo, Mapunda anaweza kujikuta katika mgogoro mkubwa zaidi na wajumbe wa Baraza Kuu, ikiwa atawasilisha majina ya watu walewale waliong’olewa ili wapigiwe kura kwa ajili ya kuthibitishwa. MWANANCHI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top