Miili
miwili iliyoungua vibaya iliyoopolewa katika eneo la kituo cha biashara
cha Westgate nchini Kenya siku ya Alhamisi inawezekana kwa kiasi
kikubwa ikawa ni ya magaidi walioshambulia kituo hicho, Mbunge mmoja wa
Kenya ameiambia shirika la habari la BBC.
Ndung’u
Gethenji mwenyekiti wa kamati ya Bunge inayochunguza shambulio hilo pia
amesema mwili mwingine ambao umepatikana unawezekana kwa kiasi kikubwa
ukawa ni wa mmoja wa wanajeshi.
Mamlaka ya Kenya kwa sasa inaendelea na uchunguzi wa kisayansi wa miili hiyo.
Karibu
watu wapatao 67 walifariki dunia wakati magaidi wanaodhaniwa kuwa ni wa
kundi la wanamgambo wa Al Shaabab waliposhambulia kituo hicho Septemba
21 mwaka huu.
Shambulio hilo lilisababisha eneo hilo kuzingirwa kwa siku nne ambapo pia sehemu kubwa ya kituo hicho cha biashara iliharibiwa.
Mamlaka ya Kenya imeyataja majina manne ya watuhumiwa wa shambulio hilo, japo hawajatoa ufafanuzi zaidi.
Bado
haijajulikana kama magaidi waliofanya shambilizi hilo kama walitoroka
au la na pia imekuwa ni vigumu kujua idadi ya magaidi waliohusika kwenye
tukio hilo.
Awali
maafisa wa serikali ya Kenya walisema inakadiriwa magaidi hao walikuwa
kati ya 10 na 15 lakini picha za CCTV zilionyesha magaidi wapatao wanne
tu ndo waliokuwepo kwenye tukio hilo.
Tayari
Kundi la Kigaidi la Al Shabaab limeshakiri kuwa ndilo lililohusika na
shambulio hilo kufuatia majeshi ya Kenya kwenda nchini Somalia kupambana
na kundi hilo.
Chanzo: BBC Swahili
Post a Comment