Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Rais Jakaya Kikwete amesema kuwa ni wajibu wa Halmashauri nchini kuhakikisha kuwa zinawabana wafanyabiashara kulipa kodi baada ya kununua mazao ya wakulima katika halmashauri hizo.


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA  
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa ni wajibu wa Halmashauri nchini kuhakikisha kuwa zinawabana wafanyabiashara kulipa kodi baada ya kununua mazao ya wakulima katika halmashauri hizo.
Rais Kikwete ameshangaa wakati wa ziara yake kusikia malalamiko ya viongozi wa Mkoa wa Njombe kuwa wafanyabiashara wanaonunua zao la pareto katika Mkoa huo wamekuwa wanakataa kulipa ushuru.
“Komesheni ujinga huu wa watu kununua pareto ya wakulima bila kulipa ushuru na kodi kwa Halmashauri. Mnajinyima wenyewe raslimali muhimu ya maendeleo yenu kwa kushindwa kuwalazimisha watu kulipa kodi,” alisema Rais Kikwete jana, Jumatano, Oktoba 23, 2013 mjini Njombe wakati anazungumza na viongozi wote wa Mkoa huo wakati anamaliza na kujumuisha ziara yake ya siku saba katika Mkoa huo.
Alisema Rais Kikwete: “Mtapata wapi fedha za kuendesha halmashauri zetu kama mnashindwa kutoza kodi na ushuru kwa watu wanaofanya biashara.  Hakuna Serikali duniani inayoendeshwa bila kutoza kodi. Hakuna. Haipo duniani.”
Rais Kikwete amesema: “Kwa kuwatoza wafanyabiashara wakubwa wanaonunua mazao kodi kunazisaidia Halmashauri na hata Serikali Kuu kuondokana na ulazima wa kuwatoza wananchi wa kawaida kodi ndogo ambazo sisi tunaziita kodi za kero na tumezifuta.”
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
24 Oktoba, 2013
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top