Mkuu
wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo akitoa ripoti fupi mbele ya wajumbe
wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Wizara ya Nishati na Madini juu ya
miradi inayotekelezwa na Wakala wa Umeme Vijijini walipomtembelea
ofisini kwake ili kuelezea nia yao ya kufanya ziara katika mkoa huo.
Wajumbe
wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Wizara ya Nishati na Madini wameanza
ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na wizara hiyo
kupitia Wakala wa Umeme Vijijini (REA) katika mikoa ya kanda ya ziwa.
Wakiongozwa
na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Victor Mwambalaswa, kamati hiyo
ilipata nafasi ya kupokea taarifa fupi kuhusu utekelezwaji wa miradi
hiyo iliyosomwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo
ambaye aliwaeleza namna sekta hiyo inavyochangia katika kuinua vipato
vya wananchi na taifa kwa ujumla.
Akitoa
taarifa kuhusu mahitaji ya umeme Mkoani humo alieleza kuwa kiasi cha
juu kinachotumiwa na mkoa huo ni megawati 46 na kuongeza kuwa , kiasi
hicho kinaonesha mahitaji halisi na umuhimu wa nishati hiyo na namna
umeme unavyochangia ukuaji wa uchumi mkoani humo.
Akizungumza
kuhusu ujenzi wa miundombinu ya umeme, alieleza kuwa ujenzi huo
umeshika kasi na kuongeza kuwa tayari tayari mradi uliotekelezwa na
Millenium Challenge Corporation (MCC) umekamilika wakati miradi
mingine inayotekelezwa na REA na Electricity Five inaendelea ambapo
takribani wilaya 9 za mkoa wa mwanza zimeguswa na miradi hiyo.
Aidha
alisema mradi wa REA phase 1 unajegwa na mkandarasi toka Symbion
umegusa wilaya ya Sengerema, Magu na Ukerewe, REA awamu ya pili utaigusa
wilaya za Magu, Misugwi, Ukerewe, Sengerema na kwimba na kumalizia kwa
mradi wa electricity five unaofadhiliwa na Benki ya Maendeleo Afrika
kuwa unagusa wilaya za Magu, Misubwi, Kwimba, na Sengerema ambapo
alisema katika mradi huo ulipwaji wa fidia kwa wananchi watakaoathirika
umeshaanza.
‘‘Kazi
ya usambazaji wa umeme Mkoani Mwanza inakwenda vizuri, kukamilika kwa
miradi hii kutasaidia vijiji vingi kuwasha umeme hivyo kukuza pato la
taifa’’ alisema Ndikilo.
Alimalizia
kwa kuwataka wajumbe hao kuwafahamisha wananchi kutumia vipato na akiba
zao katika kujenga nyumba zenye ubora ili waweze kuunganishwa na
huduma ya umeme.
Vilevile
Mhe Ndikilo aliwaomba wajumbe kuwaeleza wananchi wanaowahudumia kujenga
mazoea ya kuwa na mwamko wa kupokea na kupenda maendeleo yanayopelekwa
kwao na serikali.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa Kamati jhiyo Mhe. Victor Mwambalaswa akipokea
taarifa hiyo alieleza kuwa nia ya serikali ni kuhakikisha kuwa idadi ya
watu waliounganishiwa umeme inapanda toka asilimia 14 hadi kufikia
asilimia 30 ifikapo 2015.
Post a Comment