Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TAKUKURU KUTOA MAFUNZO KWA MABARAZA YA MADIWANI


mkuchika-june24-2013 2e521

Waziri wa nchi ofisi ya Rais anayeshughulikia Utawala bora Kepteni Mstaafu George Mkuchika ameziagiza Halmashauri na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kutoa mafunzo ya jinsi ya kupambana na rushwa kwa mabaraza ya madiwani nchini.


Akizungumza kwenye kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa wa Iringa kilichofanyika kwenye ukumbi wa Siasa ni kilimo Mkuchika alisema mafunzo hayo yanatakiwa yafike mpaka kiwango cha kata ili kuongeza chachu ya mapambano ya rushwa nchini.


Alisema mafunzo hayo yanatakiwa kufika mpaka kiwango cha madiwani kwa kuwa ndio wao wanaoishi na wananchi na miradi mingi ya maendeleo inafanyika huko.

Mkuchika alisema jukumu la kuzui na kupambana na rushwa siyo la serikali peke yake bali ni la kila mwanajamii, taasisi za umma, taasisi binafsi, jumuiya za kidini pamoja na washirika wengine wa maendeleo wa kimataifa.

Alisema ni wazi kuwa rushwa ni kikwazo kikubwa katika cha uwepo wa utawala usio bora katika nchi yoyote Duniani na dawa sahihi ya kudhibiti ni kila mmoja kuzingatia maadili.


Aliongeza kuwa hatua hiyo itaiwezesha serikali kutekeleza majukumu yake ipasavyo na pia wananchi kupata huduma bora kwa wakati na kuwa na maendeleo tarajiwa ya kiuchumi, kisiasa na kijamii katika mkoa wa Iringa.


Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa, Stephen Mhapa alisema ni vema mafunzo kama hayo yakafika mpaka kwa wananchi wa kawaida ambao ndio waathirika wakuu wa tatizo la rushwa badala ya kuishia kwenye mikoa na wilaya tu.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa, Aman Mwamwindi alisema mafunzo hayo ni muhimu na kuwa Halmashauri yake kjwa kushirikiana na kamanda wa TAKUKURU kwa kutumia bajeti yao finyu watafanya mafunzo hayo kwa madiwani. Chanzo: Hakimu Mwafongo


Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top