Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

AZAM FC MABINGWA 2013/2014, WAINYUKA MBEYA CITY 2-1, YANGA YASHINDA 2-1!

 


AZAM SHANGILIA2
RASMI Azam fc wamefanikiwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu sokA Tanzania bara msimu wa 2013/2014 baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mbeya City FC kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Kwa matokoe hayo, Azam fc wamefikisha pointi 59 kileleni ambazo haziwezi kufikiwa na klabu yoyote ile, huku wakiwa na mchezo mmoja mkononi.
Taarifa kutoka Mbeya zinaeleza kuwa mechi iliingia dosari baada ya wachezaji wa Mbeya City kumshambulia mwamuzi kutokana na kutoridhishwa na maamuzi yake.
Mtandao huu unafuatilia kwa kina kujua nini kilichosababisha tafrani hizo na baadaye utapata taarifa rasmi.

Mbeya City baada ya kuchapwa leo hii, wanabakia katika nafasi ya tatu kwa pointi 47.

Rasmi wameshajiengua kutafuta nafasi ya pili kwasababu hata kama watashinda mechi yao ya mwisho dhidi ya Mgambo JKT aprili 19 watafikisha pointi 50 ambazo zimepitwa na Yanga.
Kwa mazingira hayo, Mbeya City wameshika nafasi ya tatu, Yanga ya pili na Azam fc ni mabingwa wapya.
Yanga waliokuwa wanafukuziana na Azam fc kuwania ubingwa wameshinda mabao 2-1 dhidi ya JKT Oljoro katika dimba la Shk. Amri Abeid jijini Arusha, lakini ushindi huo haujawasaidia chochote kutokana na ushindi wa Azam fc 
Na Baraka Mpenja wa fullshangwe, Dar Es Salaam
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA CHINI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top