Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

CHEKI JINSI SIMBA ALIVYOMUUA MAMA WA NYANI NA KUMLEA MTOTO WA NYANI

 




Simba akiwa amembeba nyani baada ya kumuua, huku mtoto wa nyani akiwa amemkumbatia mama yake bado.



Muda mfupi, mtoto wa nyani alitaka kutoroka lakini alishindwa kupanda mti, sasa simba akamfuata kuona nini kinaendelea.


Lakini cha ajabu badala ya simba kumuua mtoto huyo wa nyani alianza kucheza naye na kukafanya kanyani kasahau machungu.


Hapa sijui nyani mtoto anawaza nini, weee usicheze na simba jamani.



Wacha weee, sasa hapa simba sijui ndo kamsamehe kweli huyu nyani au ndo amemuweka kiporo njaa ikiuma amtafune, lakini mtoto wa nyani anaonekana kuenjoy tu.



Nyani mtoto kashapagawa na joto la simba, anaanza kutafuta kunyonya kifuani kwa simba, ana hatari huyu mtoto.

Raha iliyochanganyikana na hofu, hatari tupu....


Wasije simba wengine! simba jike akaanza kuwatimua sasa sijui alikuwa anakalinda katoto ka nyani kasiliwe au aliona wenzake watammalizie msosi wake wa baadae.



Stori hii ni ya kufurahisha, huzunisha na kushangaza na inaonyesha ni kwa kiasi gani kila jambo limepangwa kwa maksudi yake na kwamba hata tukiwa katika magumu ya hali gani ukombozi unaweza kupatikana kikubwa tu ni kujiamini kama mtoto wa nyani alivyofanya.


Haa! kumbe baba nyani alikuwa kando akifuatilia issue yote na wakati simba wanazinguana akapata upenyo wa kumuokoa mwanaye na kupanda nae kwenye mti, uuuh kweli kama siku yako haijafika unaweza hata kumkamua maziwa simba na akabaki kukuchekea tu.
 
**********************************************************
Mpiga picha Evan Schiller na Lisa Holzwarth wametumia muda wao wa kutosha tu kuchukua picha za tukio la kusisimua na kusikitisha huko Botswana baada ya kushuhudia nyani mwenye mtoto akikumbana na hasira za simba jike mwenye njaa ambaye alimfukuza na hatimaye kumkamata na kumuua.

Nyani huyo aliuawa huku mtoto wake mchanga akiwa amemkumbatia pasipokujua kuwa mama yake tayari alikuwa ameshakufa. baada ya simba kuua nyani huyo sasa kibao alikigeuzia kwa mtoto ambapo aliaanza kumtisha pamoja na mtoto huyo wa nyani kutaka kukimbia simba alimkamata tena.


Habari Picha kwa hisani ya tabianchi blog
 
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top