|
Waumini
wa kanisa la Wadventista wa Sabato Jimbo la Nyanda za juu kusini
mkoani Mbeya limetoa msaada wa vitu mbali mbali kwa wafungwa wa gereza
la Ruanda jijini hapa.
Akizungumza
na waandishi wa Habari katika Hafla ya kukabidhi zawadi hizo kwa niaba
ya Askofu Joseph Mngwabi, Mkurugenzi wa Afya na Mawasiliano Jimbo la
Nyanda za juu kusini wa Kanisa la Sabato, Mchungaji Haruni Kikiwa,
amesema ni sehemu ya kutimiza neno la Mungu.
Amesema
msaada huo umetolewa na kanisa pamoja na waumini waishio ndani na nje
ya nchi ambao wametoa zawadi mbali mbali ambazo zitanufaisha Gereza zima
zenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 3.7.
Amezitaja
zawadi hizo kuwa ni pamoja na vyakula na matunda vyenye thamani ya
shilingi Milioni 2,027,000 Nguo shilingi 240,000 na vitabu vya dini 525
vyenye thamani ya shilingi million 1.3 ambavyo vilikabidhiwa gerezani
hapo na kufuatiwa na ibada ya kawaida.
Kwa
upande wake Mchungaji Eliot Kiswaga ambaye ni mkufunzi wa dini Gerezani
hapo amesema ni vema taasisi zingine za kidini na mashirika binafsi
yakajitoa kwa ajili watu wenye mahitaji kama wafungwa kwa kutoa misaada
mbali mbali ili kuwatambua kama jamii ya kawaida.
Naye
muumini wa Kanisa hilo, Tully Musyani, amesema kama waumini wa Kanisa
la Wadventista wa sabato wanaguswa sana na binadamu wenzao wanaotumikia
vifungo magerezani hivyo njia ya kuwafariji katika shida hizo ni kutoa
misaada ya hali na mali.
Amesema
kanisa kupitia kwa waumini wao na marafiki wanaoishi nje na ndani ya
Nchi wameitikia wito wa kutoa vitu mbali mbali ili kuwafariji wafungwa
gerezani pamoja na kutoa pongezi kwa Wahitimu wa mafunzo ya neno la
Mungu yaliyotolewa na Chuo cha Sauti ya unabii chenye makao makuu mkoani
Morogoro.
Mafunzo
hayo yamewanufaisha Wafungwa 262 na Askari 20 wa Jeshi la Magereza wa
Gereza la Ruanda mkoani Mbeya wamehitimu mafunzo ya Biblia yaliyotolewa
na Chuo cha sauti ya unabii kinachomilikiwa na Kanisa la Wadventista wa
Sabato nchini.
Mwisho.
|
on Monday, April 21, 2014
Post a Comment