Baadhi ya wanawake wanapinga sheria inayoruhusu wanaume kuoa mke zaidi ya mmoja
Sheria inayoruhusu wanaume kuoa wake zaidi ya mmoja, imepitishwa nchini Kenya.
Rais Uhuru Kenyatta ametia saini sheria hio licha ya malalamiko kutoka kwa vikundi vya wanawake nchini humo.
Taarifa
kutoka katika ofisi ya Rais ilisema kuwa mswada huo ambao unaojumuisha
vipengee kadhaa kuhusu ndoa , imekuwa sheria sasa. Mswada huo ulioleta
mageuzi katika sheria ya sasa , ilipitishwa na bunge mwezi jana
kuidhinisha rasmi utamaduni wa ndoa ya zaidi ya mwanamke mmoja

Wabunge wanaume waliungana licha ya vyama vyao kupitisha mswada huo
Taarifa
ya Rais ilisema kuwa "ndoa ni muungano wa watu wawili mwanamke na
mwanamume , ikiwa mume atataka kuoa mke mmoja au wawili, mwenyewe
anapaswa kuamua. ''
Mswaa
wa awali, ulimpa mwanamke haki ya kwenda mahakamani kupinga mume wake
kuoa mke wa pili, lakini wabunge wanaume waliungana katika kuunga mkono
mswada huo.
Wakati mswada huo ulipopitishwa mwezi jana , wabunge wanawake waliondoka bungeni kwa Hasira baada ya mjadala mkali.
Viongozi wa baadhi ya makanisa pia wamepinga vikali mswada huo
Shirikisho la kitaifa la mawakili wanawake pia limesema kuwa litapinga sheria hiyo mahakamani.
Katika
sehemu nyingi barani Afrika, kuoa zaidi ya mwanamke mmoja ni jambo la
kawaida katika tamaduni nyingi sawa na hali ilivyo nchini Kenya na hata
pia miongoni mwa waumini wa dini ya kiisilamu.
Wengi wanasema kuwa sheria hiyo inapiga tu muhuri wa utamaduni uliop


Post a Comment