Baadhi
ya wahariri na waandishi wa Magazeti ya Mtanzania, Bingwa, Dimba, Rai
na The African, Mwani Nyangasa na wenzake wakila Ndizi kwa pamoja kama
ishara ya kumuunga mkoni mchezaji wa Barcelona Mwafrika aliyeonyeshwa
vitendo vya ubaguzi wa rangi hivi juzi wakati akiwa mchezoni na timu
yake ilipokuwa ikicheza, ambao mashabiki walimrushia ndizi mbivu
uwanjani na yeye kwa kuwaonyesha kuwa hajali kitendo hicho aliiokota na
kuimenya kisha kuanza kuila, jambo ambalo liliungwa mkono na wengi na
kumpongeza kwa kitendo chake cha ujasiri, na kuendelea na mchezo.
Baloteli
pia ni mmoja kati ya wachezaji Waafrika aliyeunga mkono kitendo cha
mwafrika mwenzake kuwakebehi na kuwadharau mashabiki hao wa ubaguzi. Na
pia Baloteli ni mmoja kati ya wachezaji wanaokumbana na vitendo hivyo
vya unyanyasaji uwanjani mara kwa mara.






Post a Comment