Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KINANA: WABUNGE WATAKIWA KUTATHIMINI VAT

               

 

abdurahman-kinana_e2b1d.png 
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimetaka wabunge wake, kuhakikisha wanafanya tathmini na kupitia upya Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na kuweka viwango vya tozo hiyo, kulingana na huduma inayotolewa kupunguza malalamiko ya wananchi.
Hayo yalisemwa mjini hapa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana, alipotembelea mradi wa ujenzi wa nyumba 60 za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika kijiji cha Inyonga wilayani Mlele mkoani Katavi.(Martha Magessa)
Viongozi wa shirika hilo, walimlalamikia kiongozi huyo wakitaka asaidie kodi ya asilimia 17, inayotozwa kwa kila nyumba za shirika hilo ipunguzwe kulingana na matumizi yake, gharama za uuzaji wa nyumba hizo nayo ipungue na wananchi wengi waweze kuimudu.
Akijibu hoja hiyo, Kinana alisema wakati umefika kwa Serikali kuanza kupitia sheria zake zinazoleta migogoro katika jamii ikiwemo sheria hiyo ya VAT, ambayo kwa sasa inatoza kila kitu kwa asilimia 17 bila kujali aina ya huduma inayotolewa.
“Ziko nyumba kweli za kutozwa kodi kubwa kama vile zile za biashara, au kampuni za madini, gesi na mahoteli makubwa, lakini nyumba hizi za wananchi wa chini nazo kutozwa VAT ya asilimia 17 ni uonevu, nitafuatilia ili hili nalo lishughulikiwe,” alisisitiza Kinana.

Akiwasilisha taarifa ya mradi huo wa ujenzi wa nyumba 60 katika Wilaya ya Mlele, Meneja wa NHC katika mikoa ya Katavi na Rukwa, Nehemia Msigwa, alisema tayari shirika hilo limeanza ujenzi wa nyumba hizo katika eneo la ekari nane lililonunuliwa kwa thamani ya Sh milioni 19.
“Huu ni mwendelezo wa utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2010 ambayo inalitaka shirika hili kujenga nyumba 15,000 hadi kufikia mwakani, hadi sasa lengo hili tumelitekeleza kwa asilimia 90 na tunauhakika hadi ifikapo mwakani tutakuwa tumefikia lengo,” alisema Msigwa.
Alisema ujenzi wa nyumba hizo ambao utachukua muda wa miezi nane, ukikamilika, nyumba hizo zitauzwa kwa viwango tofauti ikiwemo gharama za juu, kati na bei nafuu ili wananchi wengi waweze kumudu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top