Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

'UKAWA WANAANDAMWA NA MIZIMWI'

               

                                          

bungemaalumkatiba_300_181_8e48d.png
MJUMBE wa Bunge Maalumu la Katiba, Zarina Madabida amesema kitendo cha wajumbe wenzao wa Bunge hilo wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kutoka bungeni juzi kinaashiria mizimu ya waasisi waliowafanyia dhihaka, inawafuatilia.
Madabida alisema jana akichangia mjadala wa Rasimu ya Katiba, sura ya kwanza na ya sita mjini hapa kuwa, ni fedheha kubwa kuwakashifu waasisi wa Taifa la Tanzania na kwamba, hali haiwezi kuwa shwari kwa waliofanya kitendo hicho.

“Walianza na Hati ya Muungano, sasa imepatikana wameanzisha chokochoko nyingine, hapa niseme ‘maweeeee’, Katiba itapatikana kwa udi na uvumba, haya yote ni mizimu ya wakubwa waliowafanyia dhihaka,” alisema Madabida.
Alisema ni bora wajumbe hao wakapata aibu kuliko fedheha, wakaamua kurejea katika Bunge ili kuonesha uzalendo wa kweli na kuandika Katiba kwa maslahi ya Watanzania.
“Rudini muombe msamaha Watanzania kwa kitendo chenu hicho, rudini tutunge Katiba,” alisema Madabida.
Mjumbe huyo alishangaa kitendo cha mjumbe Profesa Ibrahimu Lipumba, kuzungumza kile alichodai uchochezi na ubaguzi ndani ya Bunge na kudai kwa mtu anayeheshimika ndani na nje ya nchi kama Lipumba, hakupaswa kufanya alichofanya.
Profesa Lipumba juzi, alipojadili kuhusu Rasimu hiyo, alisema kumekuwa na vitendo vya ubaguzi, matusi na vitisho huku akimtaja Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi kuwa alitoa hotuba ya uchochezi na vitisho kwamba jeshi litachukua nchi ikiwa serikali tatu itapitishwa.
Alisema Lukuvi alifanya hivyo na kushawishi wananchi waunge mkono serikali mbili Jumamosi iliyopita katika Kanisa la Methodist mjini hapa kwenye Ibada ya kumsimika Mchungaji Joseph Bundala kuwa Askofu.(Martha Magessa)
Lukuvi alimwakilisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Baada ya kujadili hotuba ya Lukuvi, Profesa Lipumba aliwaongoza Ukawa wote na baadhi ya wajumbe wa kundi la 201, kutoka nje ya ukumbi wa Bunge.
“Mtu mwenye ghariba kama Profesa Ibrahimu Lipumba kufanya uchochezi alioufanya hapa jana (juzi), kuanza kugombanisha Watanzania ni hatari sana,” alisema Madabida.
Naye Mjumbe Dk Christine Ishengoma aliungana na Madabida kuwataka wajumbe hao kurejea bungeni ili kutengeneza Katiba. Hoja ya kuwataka warudi, ilitolewa pia na Mjumbe mwingine Athuman Mfutakamba akiwataka warudi bungeni na kuridhia ukweli kwamba wananchi wanataka muundo wa serikali mbili na si vurugu.
CHANZO:HABARILEO 
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top