Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Kisa Gonjwa La Ajabu, Atembea Kwa Mikono Na Miguu





Mzee Petro Bulimi akiwa nyumbani kwake.  
Mzee mwenye miaka 72, Petro Bulimi  mkazi wa Kijiji cha Itwimila A, Wilaya ya Magu mkoani Mwanza anatembea kwa kutumia mikono na miguu kufuatia kusumbuliwa na tatizo la uvimbe katikati ya uti wa mgongo. Ugonjwa huo pia umesababisha kuibukwa kwa magonjwa mengine kibao yakiwemo ya miguu kuchezacheza  kama kuna golori ndani yake zinazozunguka.
Matatizo hayo yamesababisha mzee Petro kushindwa kutembea kama binadamu wengine! Ama kweli hujafa hujaumbika!

Mzee Petro Bulimi akitembea kwa kutumia miguu na mikono akiwa nyumbani kwake.

Akisimulia kwa uchungu huku akiwa ameshika sikio moja ili apate uelekeo mzuri wa mawimbi ya sauti, mzee huyo alisema alianza kuumwa mwaka 2007 kwa kuvimba tumbo na kuwa kama mama mjamzito, baadaye alipelekwa Hospitali ya Mkoa wa Mwanza, Sekou Toure ambapo ugonjwa haukupatikana.
Mwaka 2008, alisema mzee huyo, alipata kizunguzungu kikali ambacho kilitibiwa kwa dawa za kienyeji na kupona ila bado mwili haukurudi katika hali ya kawaida kwa tumbo kuvimba.
Alisema mwaka 2009 alipelekwa Hospitali ya DDH wilayani Bunda, Mara ambako vipimo vilionesha kuwa, ana TB ya mifupa, alipatiwa dawa na kurudi nyumbani.

Nyumba anayoishi mzee Petro Bulimi  mkazi wa Kijiji cha Itwimila A, wilaya ya Magu mkoani Mwanza.

Baada ya miezi 6 alipona TB, lakini ndipo ukawa mwanzo wa miguu yake kupooza na kukosa nguvu. Hakuweza kusimama tena  kama zamani, muda mwingi aliutumia kulala na kukaa kwenye kiti cha kuegamea na alipotaka kutoka sehemu moja kwenda nyingine alitumia na mikono (angalia picha).
Mzee Petro aliendelea kusema kuwa, uliibuka uvimbe katikati ya uti wa mgongo uliomsababishea kupinda kwa mgongo.
Mzee Petro alisema ameshahangaika sana kutafuta tiba lakini wapi! Amefikia hatua ya kukata tamaa kwa sababu sehemu nyingi za tiba akienda anaambiwa atoe shilingi 250,000 kwa ajili ya dawa.
Aliongeza kuwa, maisha yake yamekuwa magumu sana kutokana na maradhi yaliyomkumba ambayo anaamini kama atapata tiba ya uhakika atapona.
“Kwa sababu nashindwa kutembea, nitashukuru sana kama nitapata baiskeli ya kukalia (wheel chair) kwa sababu itanisaidia kutembelea kwa muda huu ninaosubiri kufa,” alisema mzee huyo.
Kwa Watanzania walioguswa na tatizo la mzee Petro wanaweza kumsaidia kwa kutuma fedha kupitia namba 0753 489614, Emmanuel Nhambi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top