Timu
ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itacheza mechi ya kirafiki na
Burundi (Intamba Mu Rugamba) Aprili 26 mwaka huu ikiwa ni sehemu ya
maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Taifa
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari ipo kambini
Tukuyu mkoani Mbeya ikijiandaa kwa ajili ya mechi hiyo ikiwa na
wachezaji waliopatikana katika programu maalumu ya kusaka vipaji.
Baadaye
wachezaji wengine wa Taifa Stars ambao wapo nje ya programu ya kusaka
vipaji wataungana na wenzao kabla ya kutengeneza kikosi cha mwisho
kitakachoivaa Burundi.
Mechi
hiyo itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itachezeshwa na
waamuzi wanaotambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu
(FIFA) kutoka nchini Kenya.
Post a Comment