Fabregas,
katika akiwa na jezi yake mpya ya chelsea baada ya kusaini mkataba wa
miaka mitano, kulia wakati akiwa arsenal na kushoto sasa akiwa na timu
ya taifa ya hispania ambao ndiyo mabingwa watetezi wa kombe la dunia.
Hatimaye Cesc Fabregas amerejea England tena jijini London ambako amesaini mkataba wa miaka mitano kuichezea Chelsea.
Chelsea ya Jose Mourinho imetoa kitita cha pauni milioni 30 kumnasa Fabregas kutosha Barcelona.
Kiungo
huyo wa zamani wa Arsenal amekubali kutua Chelsea chini ya Jose
Mourinho na amesema alitamani kuichezea klabu hiyo tokea akiwa
mdogo. "Niliona bado sijamaliza kazi England, nimeamua kurudi na
ninataka makombe tena. "Najua Chelsea ina wachezaji bora na meneja wa
kiwango cha juu kabisa. Nimefurahi sana," alisema Fabregas ambaye sasa
yuko na Hispania inayopambana kutetea ubingwa wake wa dunia nchini
Brazil.
|
Post a Comment