Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Jeshi la Polisi laanza kuwasaka waliohusika na mlipuko wa bomu huko Zanzibar ambapo mtu mmoja amefariki na wengine 7 wamejeruhiwa


Wakazi wa Zanzibar wako katika hali ya wasiwasi baada ya  kushuhudia tukio lengine la  kulipuka bomu kwa viongozi wa dini huku safari hii likiua kijana mmoja na kujeruhi saba.
 
Kwa mujibu wa mkurugenzi wa upelelzi na makosa ya jinai zanzibar Sacp Yussf Ilembo,  bomu hilo lilitupwa na mtu au watu wasijulikana ambao walikuwemo ndani ya gari lilkuwa halina  namba za usajili ....
 

Ilembo  amesema  kuwa  bomu  hilo lilitupwa kwa kikundi cha wananchi waliokuwa pamoja na viongozi wa dini ambao walikuwa wametoka msikitini na wamesimama nje ya gari.
 
Kijana mmoja Mohamed khatibu Mkombalaguha ambaye ni mkaazi wa pongwe Tanga aliyekuja Zanzibar kwa ajili ya hitima alifariki hapo hapo na wengine saba akiwemo Sheik Kassim Mafuta wamejeruhiwa... 
 
Nao baadhi ya majeruhi Ahmed Haidar na mwanawe khalid Ahmed wakiongea  wakiwa wamelazwa hosptali ya Alrahma wamesema hawajui wala hawakumuona mtu ailyerusha bomu hilo, wao wameshtukia  mlipuko mkubwa .
 

 Mkurugenzi  huyo  wa Upelelezi na Makosa ya Jinai Zanzibar  amesema kuwa jeshi la Polisi limeanza kuwasaka waliohusika na mlipuko wa bomu hilo.

source: TBC
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top