Gari la Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, yenye namba T 862 BBC aina ya JEEP, imepata ajali jana mchana katika maeneo ya Nyasubi Kahama, kwenye barabara kuu iendayo nchi jirani za Rwanda na Burundi.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga Khamis Mgeja |
Kwa
mujibu wa taarifa kutoka eneo la tukio, mara baada ya ajali hiyo dereva
wa gari hilo ambaye hajafahamika mara moja alikimbia, huku ikiarifiwa
kuwa alipata majeraha kidogo kwani gari liliangukia upande wake.
Mtu
mwingine ambaye alikuwepo katika ajali hiyo hakupata majeraha yoyote,
na kwamba Gari hiyo imeinuliwa na kuondolewa eneo la tukio.
Akizungumza
kwa njia ya simu Mwenyekiti huyo wa ccm mkoa wa
Shinyanga Khamis Mgeja amesema yeye hakuwemo katika gari hilo
Gari hiyo muda mfupi baada ya kuinuliwa kutoka mtaroni |
Credit: na Malunde1 blog
on Monday, June 16, 2014
Post a Comment