Wasomi
wanapokutana hasa katika zoezi la kutunukiwa cheti kama kielezo cha
uhitimu wa ngazi fulani kuna vitu huwezi kuvifikiria kama vitatokea hata
kidogo.
Katika Jack Britt High School, North
Carolina, Marekani wanafunzi mmoja amewaacha hoi mamia ya watu
waliohudhuria sherehe ya kutunukiwa vyeti (graduation) baada ya kupanda
jukwaani kupokea cheti chake na ghafla akavua johon lake na kubaki na
boxer.
Baada ya kuvua joho alinyoosha mikono
yote miwili juu kama mwanamieleka anayetamba. Lakini haikuchukua round
wanausalama wakamdhibiti na kumuweka chini ya ulinzi.
Kwa mujibu wa The Huffington Post, kijana huyo alinyang’anywa diploma yake na hivyo hakukabithiwa cheti.
Hata hivyo bado anahesabiwa kama mtu aliye maliza masomo yake na kuhitimu licha ya kuwa hana kielelezo cha elimu yake.
“Shule yetu imefanya jitihada kubwa.
Hapo zamani watu waliohudhuria walikuwa wenye vurugu wakati wa
graduation. Tumefanya jitihanda kuwafanya watu waheshimu wanafunzi. Huyu
kijana amechagua kutoonesha heshima kwa wanafunzi wenzake.” Alisema Dr
Frank Till, mwalimu wa chuo hicho.
Post a Comment