Mchungaji Langeni Mwasibira wa Baptist Church lililopo Kyela mkoani Mbeya amelazimika kuondoka hospitalini Muhimbili jijiniDar es Salaam kurejea nyumbani baada ya kuambiwa ugonjwa wake hautibiki.
Mchungaji Langeni Mwasibira (39) wa Baptist Church lililopo Kyela mkoani
Mbeya amelazimika kuondoka hospitalini Muhimbili jijini Dar es Salaam
kurejea nyumbani kusubiri kufa baada ya madaktari kumweleza wazi kuwa
ugonjwa wake hauwezi kutibika.Gazeti hili liliwahi kuandika habari za
Mchungaji huyo katika toleo namba 842, wakati huo waumini wake
walipoamua kufunga na kumfanyia maombi kutokana na hali yake kuzidi kuwa
mbaya.
Mchungaji
huyo ambaye ni mkazi wa kijiji cha Kisyosyo kata ya Matema, Kyela
anasumbuliwa na ugonjwa ujulikanao kwa jina la Nerofibroma, alisema
anafanya utaratibu wa jinsi ya kuondoka kwenda kwao.
Mchungaji Langeni Mwasibira akiwa katika hospitalini ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam.
“Nimeteseka
kwa muda mrefu sana bila kupata nafuu, gonjwa hili lilinianza mwaka
1994 kama doa jeusi, baadaye ukatokeza upele, nilipoenda hospitali yetu
ya wilaya ya Kyela hawakugundua tatizo, ilibidi niende hospitali ya
rufaa ya Mbeya mwaka 1998.
“Katika
hospitali hiyo nayo walishindwa, hawakuniambia kinachonisumbua, uvimbe,
muwasho na maumivu makali yaliongezeka, ilibidi walipasue lakini
hakukuwa na nafuu, bali ndipo ulizidi kuumuka na maumivu yasiyo na
kifani.”
Kwa walioguswa na habari hii wanaweza kuwasiliana au kumsaidia mchungaji kupitia namba zake ambazo ni 0758 902884 au 0786 557612
Post a Comment