Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Uamuzi wa Serikali waingia utata

         

           
Chumba cha maabara
********
Wakati sekta ya afya ikikabiliwa na upungufu wa wataalamu, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imesitisha ajira za wataalamu 204 wa maabara walioajiriwa mwishoni mwa mwaka jana kwa madai kuwa hawana vigezo vya kufanya kazi katika maabara za binadamu.
Watalamu hao waliohitimu kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) pamoja na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), wamefanya kazi kwa kipindi kisichozidi miezi sita kabla ya ajira zao kusitishwa.

Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa kikao cha kusitisha ajira za vijana hao kilifanyika Januari, kati ya wizara na wawakilishi kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma.(P.T)
Serikali ilieleza wataalamu hao hawana sifa za kisheria za kuwawezesha kusajiliwa au kupata leseni ya Baraza la Wataalamu wa Maabara wa Afya nchini, bali wanatambulika kwa uwezo wao wa kufanya utafiti wa kisayansi katika maeneo husika.
Baada ya kikao hicho, Kaimu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk Donan Mmbando alitoa agizo kwa waajiri wote nchini ambao ni makatibu wakuu, makatibu tawala wa mikoa na wakurugenzi wa halmashauri za jiji, manispaa na wilaya kote Tanzania Bara kufuta ajira hizo za maofisa wa teknolojia Daraja la II.
"Kwa mujibu wa waraka huu, wanaostahili kuajiriwa kama wateknolojia daraja la II ni wenye shahada ya sayansi katika mojawapo ya fani za maabara, radiolojia, macho, viungo bandia, meno na dawa kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali na kusajiliwa na mabaraza ya taaluma," inaeleza sehemu ya waraka hiyo ya Dk Mmbando.
Msemaji wa Wizara ya Afya, Nsachris Mwamaja, alisema kuwa hakuna mabadiliko yoyote yanayoweza kufanywa baada ya maamuzi yaliyofikiwa na kikao cha Januari.
Wataalamu
Profesa Joshua Malago kutoka Sua anasema kuwa katika kikao hicho ilibainika kuwa kuna kozi mbili ambazo hazifundishwi katika vyuo hivi viwili na kwamba ndivyo vilivyowanyima wahitimu wao leseni kutoka bodi husika.
"Elimu ya wahitimu wetu iko juu sana kuliko hata wanaozalishwa katika vyuo vingine wanavyovitambua, changamoto pekee ni 'patient handling na anatomy'. Lakini tumekubaliana tuziongeze. Ni kozi rahisi kuliko ambazo tumewafundisha na zinaweza zikafundishwa ndani ya wiki mbili au tatu kama utaratibu utaandaliwa wa kuwapa 'on job training," anasema Profesa Malago.
Malago anaongeza kuwa taarifa walizozipata kutoka kwa wahitimu wao waliokuja kujiendeleza wakiwa wametoka kazini zinaeleza kuwa hawajakubaliwa na bodi za taaluma zao kusajiri vyeti vyao vya shahada.
"Wanatambulika kuwa na stashahada hata baada ya kupata shahada yetu ambayo inatambulika kimataifa," anaeleza Profesa Malago.
Chanzo:Mwananchi
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top