Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

UGONJWA WA AJABU ... AVIMBA NA KUOZA MGUUNI

Joseph Hamis Mruma akiwa na msamaria mwema anayemuuguza
Mwanafunzi (denti) wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari ya J.K.Nyerere, mkoani Kilimanjaro, Joseph Hamis Mruma (17), ameshindwa kuendelea na masomo tangu Januari, mwaka huu kutokana na maunivu makali ya donda la ajabu lililotokeza katika kisigino cha mguu wake wa kushoto.
Donda hilo amedumu nalo kwa miaka mitatu sasa na limemfanya akose raha.NI YATIMA
Joseph ni mtoto yatima, aliokotwa na msamaria mwema eneo la Himo mkoani Kilimanjaro akiwa anaokota vitu katika mapipa na mashimo ya takataka akidai hana mahala pa kuishi wala kupatia chakula baada ya wazazi wake kufariki.
MUUGUZAJI WAKE ANASEMAJE?
Muuguzaji wake anayemtunza aitwaye Conjesta Joseph Masawe anasema hivi:
“Mtoto huyu nilimuokota mtaani akiwa akitafuta chakula katika jalala maeneo ya Himo, mkoani Kilimanjaro. Wakati huo alikuwa na miaka kumi, alinieleza kuwa yupo katika mazingira hayo kutokana na tabu anayopata baada ya kufiwa na wazazi wake.
“Nilimuuliza kama ana ndugu yake alisema kwamba anaye mjomba wake ambaye alikuwa akimlea baada ya wazazi wake kufariki na aliamua kumtimua bila sababu za msingi.
“Alieleza kuwa awali alikuwa akiishi na wazazi wake jijini Dar es Saalaam maisha ya furaha.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top