Baadhi ya wajumbe wa UVCCM wakiwa na mabango yenye ujumbe wa kumpinga mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Moro Bi. Erieth Suta
Kamanda wa UVCCM akisoma moja ya mabango hayo,
Mjumbe kutoka Wilaya ya Kilombero
Kutoka wilaya ya Ulanga
Baadhi ya wajumbe hao wakiingia kwenye Kikao hicho cha baraza la Vijana mkoa kwa nyimbo na mabango ya kumpinga mwenyekiti wao
Mgeni rasmi wa Kikao hicho kamanda wa UVCCM Taifa Kingunge Ngombale Mwilu akiingia kwenye ukumbi huo wahotel ya Usambara iliyopo Nane Nane mkoani hapa
Mzee Kingule akiwa na mwenyekti wa UVCCM Mkoa wa Moro Erieth Suta (kulia)
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Morogoroo Bi,Erieth Suta anayelalamikiwa na wajumbe akidaiwa kushindwa kuiongoza Jumuiya hiyo
Mwenyekiti huyo akimkaribisha mgeni rasmi
Kamanda mkuu wa UVCCM Taifa mzee Ngombale Mwilu akizungumza kwenye Kikao hicho cha baraza la Vijana mkoa wa Moro
Mzee Kingunge kisisitiza jambo kwenye hotuba yake jana
Baada
ya kuzungumza Mzee Kingunge alisaini na kuwapa cheki ya shilingi
milioni moja akichngia mfuko wa kusaidi Vijana wa Umoja huo,
Pichani Kamanda huyo akiisaini Cheki hiyo
Akimkabidhi mwenyekiti wa UVCCM mkoa
Mwenyekiti huyo akiwaonyesja wajumbe wa mkutano huo
Makamanda wa UVCCM Kutoka Wilaya zote za mkoa wa Morogoro wakisubiri kuapishwa
Kamanda wa UVCCM Taifa Mzee Kingunge akiwaapisha makamanda hao
Wakila kiapo cha kuutumikia Umoja huo
Kamanda
mkuu wa UVCCM Taifa mzee Kingunge akimvisha Skafu kamanda wa UVCCM
Wilaya ya Morogoro Mjini Bw Paskal Kihanga ambaye pia ni mwenyekiti wa
Chama cha Soka Mkoa wa Morogoro'MRFA'
Kihanga akiwa na Mzee Kingunge baada ya kura kiapo
Na Daustan Shekidele, Morogoro
WAJUMBE
wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi'UVCCM Mkoa wa Morogoro jana
walimchana livekwa ujumbe wa mabango mwenyekiti wao wa mkoa Bi,Erieth
Suta mbele ya kamanda mkuu wa taifa wa UVCCM Kingunge Ngombale Mwilu.
Wajumbe
wa Jumuiya hiyo kutoka wilaya zote za mkoa wa Morogoro walijipanga
kwenye geti kuu la hotel ya Usambara ambapo kikao hicho cha Baraza la
Vijana mkoa wa Morogoro kilifanyika ambapo mgeni wa kikao hicho kamanda
wa taifa wa UVCCM Kingunge Ngombale Mwilu alisoma mabango hayo
alipowasili kwenye hotel hiyo.
Hata
hivyo kwenye hotuba yake kamanda huyo wa taifa hakugusi ishu hiyo na
kwamba baada ya kamandas huyo kufunga kikao hicho majira ya saa 11 jioni
aliondoka na wajumbe hao wareje kwenye kikao hicho huku ambacho watu
wote wasiokuwa wajumbe hawakutakiwa kuingia kwenye kikao hicho.
Kufuatia
hali hiyo mwandishi wetu aliwashuhudi makachelo wa Polisi wakisambaa
kwenye hotel hiyo kuimalisha ulinzi kwenye kikao hicho kilichomalizika
saa nne usiku.
Mjumbe
mmoja wa kikao hicho alimweleza mwandishi wetu kwamba wajumbe hao
wameshinda kumng'oa mwenyekiti huyo baada ya kukosa ushahidi wa tuhuma
walizoeleke kwa mwenyekiti huyo.
Post a Comment