
Msanii mkongwe wa filamu Bongo Blandina Chagula ‘Johari’
WASANII wa filamu Bongo, waliokuwa katika kamati
maalum iliyoundwa na Mwenyekiti wa Bongo Movie
Unity Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ ya kukabidhiwa
ukamanda wa vijana, juzi walimcheka mwenzao,
Blandina Chagula ‘Johari’ kwa kunyang’anywa bwana.
Tukio hilo lilitokea juzi maeneo ya
Mwananyamala jijini Dar es Salaam, ambapo wenzake walimcheka kutokana na
aliyekuwa mpenziwe, Vicent Kigosi ‘Ray’ kuporwa na mwigizaji mwenzake,
Chuchu Hans.
“Niachieni Johari wangu jamani,
mnamkerakera kila wakati hadi anakosa amani kwani wanaume wameisha
atapata mwingine” alisikika Steve Nyerere akimfariji msanii huyo mkongwe
ambaye aliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Ray.
Post a Comment