Maelfu ya watu hutoka sehemu mbali mbali za dunia kutafuta kupona katika kanisa la TB Joshua
Wanaume na wanawake waanguka sakafuni wakati wakiombewa na TP Joshua
Marais wengi Afrika wamemtembea Joshua wakitafuta kuombewa
Kanisa
lililoporomoka mjini Lagos wiki jana , na kuwaua watu wengi, lilikuwa
linamilikiwa na mhubiri anayesifika sana nchini Nigeria, TB Joshua.
Mwandishi
wa BBC Tomi Oladipo anatufichulia haiba ya mhubiri huyu ambaye anadai
amewaponya watu wakiwemo vipofu na waathiriwa wa HIV...(MC)
TB Joshua
anadai kuwahi kutabiri matukio mengi kuanzia kwa kifo cha aliyekuwa
gwiji wa muziki, Michael Jackson, hadi kupotea kwa ndege ya Malaysia ya
MH370"
Anajiita mtume na ni mmoja wa wahubiri mashuhuri sana nchini Nigeria ambako makanisa kama lake ni mengi kupindukia.
Alizaliwa mwaka 1963 tarehe 12 Juni katika familia maskini, akidai kwamba alikaa kwenye tumbo la mamake kwa miezi 15.
Baadaye katika maisha yake, anadai kuona kwenye ndoto yake manabii wakimtaka kuhubiri na kufanya miujiza.
Hapo ndipo alipoanzisha kanisa lake analoiita, 'Church of All Nations (SCOAN),' mwanzoni likiwa na waumini 8.
'Maji ya kuponya'
Wanaume
na wanawake waanguka sakafuni wakati wakiombewa na TP JoshuaHii leo
Jushua kama wahubiri wengine nchini Nigeria, ni tajiri wa kupindukia
akishabikiwa sana na watu nchini humo.
Watu huja kwake kutoka kote duniani wakitaka kuombewa wapone.
Wakati
ugonjwa wa Ebola uliporipotiwa katika kanda ya Afrika Magharibi,
serikali ya jimbo la Lagos, ilimtambua muhubiri huyo kwa kuambia
wagonjwa wa Ebola kwenda kwake akawaponye.
Alikubali
kuahirisha baadhi ya programu za kanisa lake za kuponya lakini
inaarifiwa alituma chupa 4,000 za maji ya ''uponyo' nchini Sierra Leone
anayosema kuwa yanatibu magonjwa mengi tu.
TB Joshua
anasema maji hayo ambayo yalitolewa kwa wagonjwa yakiwa ndani ya chupa
ndogo, ndogo, yanaweza kuwasaidia wagonjwa kupona na kupata baraka.
'Utabiri'
Maelfu ya
watu hutoka sehemu mbali mbali za dunia kutafuta kupona katika kanisa
la TB JoshuaAnasifika, kwa unabii wake, TB Joshua anadai kutabiri
matukio mbali mbali kuanzia kwa kifo cha marehemu Michael Jackson, hadi
kupotea kwa ndege ya Malaysia MH370.
Katika
utabiri wake wa kifo cha Michael Jackson, TB Joshua aliwaambia waumini
wake: ''Katika maeneo yake mwenyewe yeye ni mashuhuri. Najulikana kila
sehemu. ''
''Kwa
sababu mwanzo huwa naona kwamba kitu kitamfanyikia mtu flani mashuhuri,
na kitu hicho kitamalizika, ila huwa sijui tu safari hiyo itakuwa lini.
''
Baada ya
kifo cha Michael Jackson, mhubiri huyo alidai kuwa alikuwa amezungumzia
kifo cha Jackson miezi sita kabla ya kutokea kwa kifo hicho.
Wakosoaji wake wanasema matamshi na utabiri wake ni wa kubahatisha.
Lakini hili halijawakoshesha usingizi waumini wa kanisa lake.
Joshua
huandika vitabu na kutengeza kanda ambazo zinauzwa kupitia
InternetMwanasiasa wa Afrika Kusini ,Julius Malema, Rais wa Malawi Joyce
Banda, na mwanasiasa wa Zimbabwe,Morgan Tsvangirai na aliyekuwa Rais wa
Ghana John Atta Mills, ni miongoni mwa watu mashuhuri ambao
wamemtembelea.
TB Joshua ni mmoja wa wahubiri mashuhuri barani Afrika.
Baadhi ya
waumini wanadai kufaidika pakubwa kutokana na maombi yake, ni wale
wanaosema wameweza kufanikiwa kifedha, kupona na hata watu kufufuliwa.
Nabii Joshua pia anajulikana kwa kazi yake kwa jamii ambayo yeye hujitolea.
Wengi nchini Nigeria hata huhofia kukmosoa TB Joshua.
CHANZO; BBC SWAHILI
Post a Comment