Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

PIKIPIKI YAPINDUKA NA KUUA DEREVA MBEYA


Ajali ya pikipiki iliyotokea usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha Ilima, tarafa ya Pakati, tarafa ya Pakati wilayani Rungwe hapa mkoani Mbeya imesababisha kifo cha mtu mmoja aliyefahamika kwa majina ya Naseeb Langson mkazi wa Igogwe, Tukuyu.

Taarifa kutoka kwa maafisa wa  polisi zinaeleza kuwa kifo hicho kimetokea baada ya pikipiki iliyokuwa ikiendeshwa na marehemu Naseeb Langson iliacha njia na kisha kupinduka na kusababisha dereva kujeruhiwa vibaya na kufariki muda mfupi baada kufikishwa katika hospitali ya wilaya ya Rungwe kwa matibabu.
Taarifa zaidi zilizoifikia Fichuo Tz zinaeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa pikipiki na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika ya wilaya ya Rungwe.
Pamoja na hayo Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Ahmed Msangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kutoa wito kwa madereva kuwa makini wanapotumia vyombo vya moto ikiwa ni pamoja na kuzingatia sheria za usalama wa barabarani ili kuepusha ajali zinazoweza kuepukika.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top