
Meja Jenerali
Aidan Isidore Mfuse (mstaafu) enzi za Uhai wake
---
Mkuu
wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange anasikitika kutangaza
kifo cha Meja Jenerali Aidan Isidore Mfuse (mstaafu) kilichotokea tarehe
29 Oktoba 2014 katika Hospitali ya Appolo nchini India alikokuwa
akipata matibabu.
Mwili wa marehemu Meja Jenerali Aidan Isidore Mfuse (mstaafu) unatarajia kuwasili Tanzania tarehe 31 Oktoba 2014 saa 7:30 mchana na kuhifadhiwa katika hospitali kuu ya Jeshi Lugalo.
Heshima za mwisho kwa Viongozi,
Wanajeshi na Watumishi wa Umma zitatolewa katika Hospitali Kuu ya Jeshi
Lugalo tarehe 01 Novemba 2014, kuanzia saa 4.00 hadi saa 5.00 asubuhi na
mwili wa marehemu utasafirishwa kwenda Njombe kwa mazishi, ambapo
mazishi yanatarajiwa kufanyika tarehe 02 Novemba, 2014 saa 8.00 mchana.
Imetolewa na
Kurugenzi ya Habari na Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga


Post a Comment