Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAKUBWA: ISHU YA WALIMU KUWAPA MIMBA WANAFUNZI WAO YAGEUKA TISHIO


KESI za kulawiti watoto mashuleni imeelezwa kuwa wanaofanya ukatili huo wa kijinsia kwa watoto hao baadhi yao ni walimu wanaowafundisha na kwamba kutokana na walimu hao kuhitajika shuleni hapo baadhi ya uongozi wa shule umekuwa ukishindwa kuwachukulia hatua ikiwa ni pamoja na kushindwa kuripoti katika dawati hilo.

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi ambaye pia ni Mkuu wa Dawati la Jinsia mkoani Kilimanjaro Prisca Maganga aliwaambia waandishi wa habari wa mikoa ya Manyara, Tanga, Kilimanjaro na Arusha waliotembelea dawati hilo mwishoni mwa wiki kuwa kwa mwezi Januari hadi Februari mwaka huu wamepokea kesi 10 za kutelekeza familia zikiwemo kesi 2 za kubaka.

Alisema kesi mbili hadi tatu za kulawiti wanafunzi wa shule za msingi mkoani Kilimanjaro zimeripotiwa kwa mwezi Januari hadi Februari mwaka huu katika dawati la jinsia mkoani humo ambapo katika kesi 10 zilizoripotiwa katika dawati hilo zilikuwa zikiongozwa na kesi za kutelekeza familia.

“Kesi za ukatili wa majumbani kama kutelekeza familia zinaongoza kwa mkoa wetu, tunapokea kesi 10 hadi 15 kwa mwezi chimbuko likiwa ni kiuchumi na changamoto za maisha na akinamama wengi wanatelekezwa kwa sababu ya utegemezi na sababu nyingine wanaume kuwa na tamaa na kuoa mke mwingine,” Alisema mkaguzi huyo wa Polisi.

Akielezea ukatili mwingine wa majumbani, alisema wazazi wengi wamekuwa wakitoa adhabu za viboko na vipigo vinavyokithiri kwa watoto wao kwa lengo la kuwakanya kitabia bila kujua kwamba zipo sheria zinazomlinda mtoto huyo dhidi ya ukatili huo na wakati mwingine wazazi hao kulazimika kufikishwa katika vyombo vya sheria.

“Baba mmoja alikuwa akimpiga mtoto wake kwa mjeledi na kuacha alama mbaya mwilini mara kwa mara na kuathiri masomo na makuzi yake na kumpiga mama wa mtoto huyo kumbe wazazi hao ni waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi, tunashukuru walimu wa shule aliyokuwa akisoma mtoto huyo kutupa taarifa na ushirikiano hadi mtoto huyo kuendelea na masomo yake mpaka sasa,” alisema.


Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top