Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WANAWAKE JITOKEZENI KWA WINGI KUPIGA KURA - MAMA SALMA KIKWETE


X1 
Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi,CCM, Mama Salma Kikwete akiwapungia mkono viongozi na wanachama wa UWT wa Mkoa wa Mara wakati akiwasili kwenye ukumbi wa Musoma Community Centre kwa ajili ya mkutano wa ndani na wanachama hao-Octoba 3, 2015.
X3 
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizungumza na wanachama wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Mkoa wa Mara wakati alipokutana nao kwenye ukumbi wa Musoma Community Centre.
X2 
Umati wa wajumbe wa Umoja wa Wanawake (UWT) wa Mkoa wa Mara wakimsikiliza kwa makini Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (hayupo pichani) wakati alipokuwa akiongea nao Mjini Musoma.PICHA NA JOHN LUKUWI.

Na Anna Nkinda – Tarime.
 Wanawake wilayani Tarime wametakiwa kujitokeza kwa wingi kupiga kura siku ya uchaguzi mkuu utakaofanyika mwishoni mwa mwezi huu itakapofika na wachague viongozi watakaowaona wanafaa ambao watawaletea  maendeleo.

Rai hiyo imetolewa leo na  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati akiongea na wanawake wa wilaya hiyo iliyopo mkoani Mara katika ukumbi wa mikutano uliopo katika hoteli ya CMG.

Mama Kikwete ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kupitia wilaya ya Lindi mjini alisema kupiga kura ni haki ya kila mtu hivyo basi haitakuwa busara kwa  wanawake hao kuharibu kura zao kwa kukaa majumbani siku ya uchaguzi ikifika bali waende kupiga kura katika vituo walivyojiandikisha .

“Kura ni siri ya mtu, wewe ndiye unayefahamu kiongozi gani wa kumchagua nawasihi chagueni viongozi wazuri na siyo bora viongozi, wahimizeni wanawake wote waliojiandikisha washiriki kupiga kura kwani kura zenu yako ndiyo itakayokupatia kiongozi unayemtaka”, alisema Mama Kikwete.

Alisema siasa siyo uadui wala ugomvi bali ni mchakato wa kidemokrasia na kuwataka wagombea wote kunadi sera zao kwa kufuata utaratibu na amani kwa kuzingatia kanuni na sheria zilizopangwa na tume ya Taifa ya Uchaguzi ili utulivu na Amani viendelee kutawala nchini.

Aliwasihi, “Msigombane kutokana na tofauti ya itikadi za vyama vya siasa, angalieni siasa zisiwafarakanishe ikafika hatua mkashindwa hata kusaidiana ikiwa ni pamoja na kushindwa kuzikana kumbukeni nyinyi ni ndugu wa wilaya moja ya Tarime”.

Aidha Mama Kikwete aliwataka  wanawake hao kujenga tabia ya  kujiwekea akiba Benki kutokana na fedha wanazozipata katika kazi wanazozifanya kwa kufanya hivyo wataweza kukopa fedha nyingi ambazo watafanyia shughuli za maendeleo na hivyo kujikomboa kiuchumi. 

“Unganeni  pamoja ili muweze kujikwamua kiuchumi, simameni katika majukwaa teteeni haki zenu, pingeni mila zilizopitwa na wakati ambazo zinamkandamiza mwanamke na hivyo kumrudisha nyuma kimaendeleo kwa kufanya hivyo mtaweza kujikomboa  kutoka katika hali ya unyanyasaji”,alisisitiza .
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top