Wasanii
wa muziki wa Dansi Bongo, Joseph Michael ‘Jose Mara’, na Charles
Gabriel ‘Chaz Baba’, Jumamosi hii (leo) wanatarajia kuirejesha bendi
yao ya Mapacha Wanne, ambayo ilikuwa ikiundwa na mastaa wenzao wawili
Khaleed Chuma ‘Chokoraa’ na Junior Kalala ‘Kalala Junior.’
Wasanii
hao usiku wa leo watafanya makamuzi ya pamoja ndani ya Ukumbi wa Mango
Garden Kinondoni jijini Dar es Salaam, ikiwa ni moja ya mwendelezo wa
kundi hilo ambalo lilisamb- aratika baada ya Chaz Baba kuzuiwa na bendi
yake ya zamani ya African Stars ‘Twanga Pepeta’, huku Kalala Junior
naye akijiengua kwenye bendi hiyo na kuwaacha Jose Mara na Chokoraa.
Akizungumza
na gazeti hili Jose Mara alisema leo watawakumbusha mashabiki zao namna
walivyokuwa wakifanya wakati wapo kwenye kundi moja, mbali na hivyo
pia itakuwa ni mwanzo wa kujenga umoja wa Mapacha Wanne, kwani
wanatarajia kupiga shoo zaidi ya moja nje ya Jiji la Dar.
“Kweli
leo Mapacha Wanne itarudi kwani tutafanya makamuzi ya nguvu hivyo
nawaomba watu waje kutushuhudia kwani tutakuwa tukitoa burudani na
kujenga umoja wa Mapacha Wanne, tutasindikizwa na Twanga Pepeta,”
alisema Jose Mara.
Post a Comment