MBUNGE
wa jimbo la Ubungo, Saed Kubenea ameibua ufisadi wa Shilingi bil. 1.2
kwa mwaka katika Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam unaofanywa kupitia
ufuaji wa majoho ya madiwani.
“Baada
ya kufanya uchunguzi tumebaini kuwa mradi huo wa ufuaji majoho kabla ya
madiwani kufanya kikao unaotumia shilingi bilioni 1.2 hivyo basi
Halmashauri ya Manispaa itakayokuwa chini ya Umoja wa Katiba ya Wananchi
(Ukawa) tukianza kazi tutaufuta,” alisema Kubenea.
Aliongeza
kuwa kufutwa kwa mradi huo kutafanywa mara moja baada ya Ukawa kupata
Meya wa Manispaa na Jiji kutokana na ukweli kwamba wana Halmashauri
mbili kati ya tatu hivyo zitawawezesha kumpata Naibu Meya katika Chama
Cha Wananchi (CUF) na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Kubenea
alisema jambo jingine ambalo watakalolisimamia ni kuhakikisha wanaondoa
Mahakama ya jiji kwa sababu wamegundua hakuna mahali popote katika bara
la Afrika.
“Mahakama
hiyo ni ya kikoloni kwani hakuna mahali popote katika bara la Afrika
ambako ipo zaidi ya Tanzania kwenye jiji la Dar es Salaam, hivyo ili
kuwaokoa mama lishe, madereva bodaboda, machinga ni lazima tuhakikishe
Mahakama hiyo tunaifuta,” alisema Kubenea.
Mbunge
huyo alisema wamedhamiria kwenda kufuta zuio madereva wa bodaboda
kuingia mjini lililokuwa limewekwa chini ya aliyekuwa Meya wa jiji, Dk.
Didas Masaburi ili kuwawezesha vijana hao kufikia katika mji huo.
Post a Comment