Polisi
mkoani Kigoma imewafukuza kazi askari wake watatu kwa kusambaza taarifa
za uongo kupitia mitandao ya kijamii juu ya utendaji kazi wa baadhi ya
viongozi wa jeshi hilo.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Ferdinand Mtui amesema kutokana na utaratibu
wa kijeshi, askari hao walichunguzwa na mashitaka yaliendeshwa dhidi yao
kwa miezi mitatu kabla ya kuchukua uamuzi huo.
Amewataja askari waliofukuzwa kazi ni Koplo Johnson, PC Justine na WP
Mercy ambao pamoja na kufukuzwa kazi, wamepewa nafasi ya kukata rufaa
ikiwa hawakubaliani na hukumu waliyopewa
Bonyeza hapa usome zaidi http://www.mwananchi.co.tz/…/1597296/2973492/-/evc69rz/-/in
Post a Comment