Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka
Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na uvuvi Bi Judith Mhina akifafanua kwa waandishi
wa habari kuhusu mradi wa udhibiti wa uvuvi na maendeleo shirikishi Kusini
Magharibi mwa bahari ya Hindi “SWIOFISH”
leo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano na waandishi wa habari. Kulia ni
Mkurugenzi Msaidizi Wizara ya Maendeleo
ya Mifugo na Uvuvi Bi Fatma Sobo.
Afisa Uvuvi kutoka
Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Bw. Silas William akitoa ufafanuzi
kwa waandishi wa habari kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali katika
kuwainua wavuvi wadogo hapa nchini ili kushiriki katika kukuza uchumi wa Taifa.
Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Wizara ya
Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Bi Fatma Sobo.mwisho kushoto ni Mkuu wa
kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na
uvuvi Bi Judith Mhina.
Baadhi ya Maafisa kutoka Wizara ya Maendeleo ya Mifugo
na Uvuvi wakifuatalia mkutano wa Wizara hiyo na waandishi wa habari uliofanyika
leo Jijini Dar es salaam.
Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya
habari wakifuatilia mkutano kati yao na Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
ambao pamoja na mambo mengine ulibainisha kuwa Serikali imejipanga kukomesha
uvuvi haramu hapa nchini hasa kwa kutumia mabomu kwa kushirikiana na Ofisi ya
Rais,Wizara ya Mali asili na Utalii, Wizara ya Nishati na Madini,Wizara ya
mambo ya Ndani na ile ya Katiba na Sheria.
(Picha na Frank Mvungi-Maelezo)
Post a Comment