Mkurugenzi
wa elimu kwa mlipa kodi kutoka mamlaka ya mapato nchini TRA Richard
Kayombo ametolea ufafanuzi juu ya kukamatwa kwa makontena 9 katika eneo
la Mbezi Tank Bovu jijini Dar es Salaam ambapo mpaka sasa hivi Makontena
hayo pamoja na madereva waliokuwa wanayasafirisha yako chini ya ulinzi
mpaka wahusika watakapojitokeza.
Kayombo
amesema kuwa makontena hayo yamenaswa usiku wa manane kwa msaada wa
wasamaria wema waliotoa taarifa za kupakiwa kwa makontena hayo katika
bandari kavu ya PMM.
Bwana
Kayombo amesema TRA imetoa masaa 24 kwa mmiliki wa makontena hayo
kujitokeza, vinginevyo watayafungua na kuyataifisha kama sheria
inavyoelekeza
Loading...
Post a Comment