Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KITLYA NA WENZAKE BADO MAMBO MAGUMU

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo imesita kutoa uamuzi wa kesi inayowakabili Harry Kitillya, Shose Sinare na Sioi Solomoni kwa madai, jalada lake limeitishwa Mahakama Kuu.

Kitillya, alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA); Sinare, Mkuu wa Idara ya Ushirikiano na Uwezekezaji katika Benki ya Stanbic na Sioi, Mwanasheria wa Benki ya Stanbic.

Amilis Mchaura, Hakimu Mkazi Kisutu amesema kuwa, hana mamlaka ya kutolea uamuzi wa kesi hiyo kutokana na jarada lake kuitishwa Mahakama Kuu leo asubuhi.

Kutokana na hali hiyo Hakimu Mchaura amesema kwamba, kesi itatajwa tena tarehe 12 Mei mwaka huu na watuhumiwa watarudishwa rumande.

Muda mfupi baada ya hakimu Mchaura kusema  hivyo, Kitilya na wenzake  walirudishwa tena mbele ya Hakimu  huyo  baada ya hakimu kupata amri kutoka kwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam akimtaka kesi hiyo itajwe Mei 3, mwaka huu badala ya tarehe 12 Mei mwaka huu aliyoipanga awali.

Hakimu Mchauru amesema, sababu za kupewa amri hiyo hazijui, hivyo kesi itatajwa tena tarehe 3 Mei mwaka huu na yale yaliyozungumzwa asubuhi yatabaki kama ilivyo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top