Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAWASILIANO BARABARA YA DODOMA NA MOROGORO YAKATIKA

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maelezo, Bi. Zamaradi Kawawa,

Mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia leo imesababisha kukatika kwa mawasiliano ya barabara kati ya Morogoro na Dodoma na kusababisha abiria wengi na magari kukwama na kushindwa kuendelea na safari zao.

Akizungumza kutoka eneo la tukio Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maelezo, Bi. Zamaradi Kawawa, amesema mawasialiano hayo yamekatika katika eneo la Chalinze Nyama ambapo abiria na magari hayo yamekwama kuanzia Alfajiri ya leo.

Bi. Zamaradi amesema mpaka sasa Askari wa Usalama barabarani wameshafika eneo la tukio kwa ajili ya kuangalia ni jinsi gani wanaweza kutatua tatizo hilo kwa haraka ili abiria waendelee na safari.

Aidha Mkurugenzi huyo amesema maji hayo yameharibu kabisa miundo mbinu katika baadhi ya maeneo na kusababisha adha kubwa ya usafiri katika Mikoa hiyo ambapo mpaka wanausalama wanaendelea na jitihada za kutatua adha hiyo iliyowakumba wananchi wengi zaidi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top