Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

BUNGE LAITAKA SERIKALI KUHARAKISHA UJENZI RELI YA KATI

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeshauri Serikali kuharakisha ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha standard gauge ili kuisaidia Bandari ya Dar es salaam kukabiliana na ushindani kutoka bandari ya nchi jirani.

Hatua hii itasaidia kuleta maendeleo ya haraka hapa nchini kupitia upokeaji na usafirishaji wa  mizigo mingi ya nchini na nje ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Profesa Norman Sigala wakati akiwasilisha taarifa kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano ya mwaka ujao wa fedha.

Amesema kuwa nchi nyingine za wanachama wa Afrika Mashariki zinaendelea kujenga reli kwa kiwango cha standard gauge kutoka Mombasa kupitia Nairobi , Kampala hadi Kigali kwa kasi kubwa.

Mhe. Profesa Norman alisema kuwa ili Bandari za Tanzania ziweze kushindana na Bandari za Kenya katika kupokea mizigo ya nchi za Uganda na Rwanda ni vema reli ya kati ikajengwa kwa kiwango cha standard gauge ili iziunganishe nchi hizo na reli inawezesha kusafirisha mizigo bila vikwazo.

Aliongeza kuwa kukamilika kwa reli kwa kiwango hicho itasaidia kuwanufaisha mikoa 15 ya Tanzania bara.

Profesa Norman alisema kuwa ni vema Serikali ikaharakisha ujenzi wa reli ya kati na matawi yake yote ambayo ni kutoka Dar salaam kwenda kigoma, Uvinza hadi Msongati kwa ajili ya mizigo ya Burundi.

Alisema kuwa tawi jingine ni lile la kutoka Tabora hadi Kalemi kwa ajili ya mizigo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) na ile ya kutoka Tabora kupitia Shinyanga hadi Mwanza kwa ajili ya Ukanda wa ziwa.

Kwa upande wa Msemaji wa Kambi Rasmi  ya Upinzani Bungeni Mhe. James Mbatia akiwalisha maoni ya Kambi hiyo alisema kuwa reli ya kati ikiboreshwa itasaidia kutawala soko la usafirishaji wa abiria na mizigo ya ndani na nje ya nchi kama vile DRC, Burundi , Uganda na Rwanda.

Alisema kuwa hivi sasa watanzania wanatakiwa kuwa na reli ambayo itaendana na hali  ya sasa inayowezesha usafirishaji wa mizigo kwa kasi na uwezo mkubwa wa kubeba mzigo mzito.

Mhe. Mbatia alishauri kuwa ili kufupisha ujenzi wa reli hiyo ni vema kukawa na wakandarasi ambao watapewa vipande vidogo vidogo vya takribani kilometa 200 ambavyo vitajengwa kwa wakati.

Naye Waziri wa Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa alisema kuwa Serikali kupitia Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli(RAHACO) inaendelea na uboreshaji wa miundo mbinu ya reli ili kuongeza uwezo wa njia zilizopo za reli ya kati za kubeba mizigo mizito zaidi.

Alisema kuwa mara baada ya kukakamilisha uboreshaji wa reli hiyo kutasaidia uhimilivu wa  mwendo kasi wa juu na kupunguza ajali za treni.

Wizara hiyo imeliomba Bunge kuidhinisha shilingi 4,895,279,317,500.00 kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu mbalimbali katika mwaka wa fedha ujao.

Kati ya fedha hizo shilingi 2,212,141,496,500.00 ni kwa ajili ya sekta ya ujenzi, shilingi 2,587,333,762,000.00 ni kwa ajili ya sekta ya uchukuzi na shilingi 95, 804,059,000.00 ni kwa ajili ya sekta ya mawasiliano.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top