Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RAIS MAGUFULI ATOA AGIZO ZITO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameyaagiza mashirika yote ya Hifadhi ya jamii kutoendelea kuwekeza katika miradi ya majengo na badala yake yajielekeze katika ujenzi wa viwanda na miradi mingine inayozalisha ajira na kuchangia zaidi katika pato Ia taifa.

Rais Magufuli ametoa maelekezo hayo leo Jumatatu tarehe 09 Mei, 2016 alipofungua majengo mawill ya vitega uchumi ya Mfuko wa Pensheni (PPF) na Shirika Ia Hifadhi ya Jamii(NSSF) yaliyopo Jijini Arusha.

Pamoja na kuyapongeza mashirika hayo kwa kujenga majengo ya kisasa jijini Arusha na maeneo mengine hapa nchini, Dkt. Magufuli amekosoa uwekezaji mkubwa unaofanywa na mashirika hayo kwa kujenga majengo ya gharama kubwa ambayo licha ya kuwa wananchi wa kawaida hawawezi kumudu gharama za kupanga kwa ajlli ya kuendesha shughull zao, hayana manufaa ya kutosha ikilinganishwa na endapo mashirika hayo yangewekeza katika miradi inayozalisha ajira nyingi, faida ya haraka na kuchangia kwa kiasi kikubwa katika palo Ia taifa.

"Hii mifuko ya hifadhi ya jamii kuanzia leo muache kuwekeza katika majengo, wekezeni kwenye viwanda, leo mngekuwa na viwanda vya sukari hawa watu wasingetuchezea kuficha sukari, na inawezekana hata kama ingepungua tungewambia nyinyi agizeni sukari.

"Mchango wa mifuko ya hifadhi za jamii katika nchi yetu, ambayo iko saba, imekuwa ikichangia pato la taifa kwa asilimia 12, lakini hifadhi ya jamii sehemu nyingine duniani, imekuwa ikichangia palo la taifa kwa asilimia 40, kwa hiyo kuna mahali tumekosea, na ndio maana mlipokuwa mkizungumza hapa sijui mlijua nitakayowaambia, ninawapongeza mliwekeza katika majengo, jengo Ia PPF na jengo IB NSSF ukipiga hesabu za kawaida haya majengo yamegharimu zaidi ya shilingi bllioni 60, lakini tujiulize hawa wananchl waliosimama hapa watayatumiaje haya majengo"Amesema Dk. Magufuli huku akishangiliwa na wananchi wa Arusha waliojtokeza kushuhudia ufunguzi huo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top