Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RUSHWA YA NGONO ADUI WA MAENDELEO

 Mratibu wa Asasi ya kuinua maendeleo ya Jamii na Kuhifadhi Mazingira (Ececo)Ndosho Hamisi akisisitiza jambo wakati akitoa mada juu ya madhara ya rushwa ya ngono iliyofanyika kijiji cha Duga wilayani Mkinga iliyokuwa na lengo la kuwapa uelewa jamii ya wasichana wa wafuigaji wa kimasaia iliyofanyika
 Baadhi ya wananchi wa Kata ya Duga Maforoni wakifuatilia mada mbalimbalio zilizokuwa zikiwasilishwa
 Katibu wa Asasi ya Kuinua Jamii na Kuhifadhi Mazingira (ECECO TANZANIA),Said Kamba akisisitiza jambo kwa washiriki wa semina hiyo
 Diwani wa Kata ya Duga Maforoni Ally Ally akizungumza katika semina hiyo

IMEELEZWA kuwa rushwa ya ngono imekuwa ni tishio hapa nchini hali inayochangia kurudisha nyuma kasi ya maendeleo kwani imekuwa ikipunguza demokrasia na utawala bora kwa watanzania jambo ambalo linapaswa kupigwa vita kwa vitendo.

Hayo yalisemwa juzi na Mratibu wa Asasi ya Kuinua Maendeleo ya Jamii na Kuhifadhi Mazingira (Ececo), Ndosho Hamisi wakati wa semina ya rushwa ya ngono iliyofanyika Kijiji cha Maforoni Kata ya Duga wilayani hapa na kufadhiliwa na Women Fund Tanzania  (WTF)iliyokuwa na lengo la kuwapa uelewa juu mambo hayo kwa wasichana na wanawake hasa wa jamii ya wafugaji wa kimasai.

Alisema kuwa tatizo hilo limekuwa likichukua kasi kwenye sekta nyingi na kusababisha kukandamiza haki za wanaostahili kuweza kupata fursa za kuweza kupata nafasi za kukuza uchumi wao na hivyo wengi wao kuishia katika hali duni.

  “Ukiangalia leo hii unaweza kutaka kitu Fulani mahali lakini kwa sababu hauna sifa ambazo zinapaswa kukipata basi yanaweza kutumika mazingira ambayo sio sahihi ili uweze kukipata kutokana na kumtimizia mahitaji yake mlengwa na hili limekuwa tatizo kubwa “Alisema.

 “Ni kosa kisheria mtu mwenye mamlaka kumpandisha cheo mfanyakazi wake kutokana na kuwepo kwa mazingira ya rushwa ya ngono kwa sababu inasababisha kupunguza ufanisi kazini na hivyo kushindwa kupiga hatua kubwa za kimaendeleo “Alisema.

Alisema jambo hilo limekuwa na madhara mengi kwa jamii ikiwemo kupata magonjwa makubwa ikiwemo ukimwi lakini pia uzalilishaji kitendo ambacho kinapelekea kushusha utendaji na kuchangia kurudisha nyuma maendeleo.

Awali akizungumza wakati akifungua semina hiyo, Diwani wa Kata ya Duga, Ally Mohamed aliipongeza asasi hiyo kwa kuona umuhimu kuwapatia mafunzo hayo ambayo yataweza kuwapa uelewa juu ya madhara ya rushwa ya ngono na kubadilika

“Unaweza kukuta wakati mwengine watoto wadogo wanazalilika kutokana na kutokujua madhara ya rushwa ya ngono hivyo semina hii itawafungua macho kuona namna ya kuweza kupiga vita vitendo hivyo “Alisema
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top