Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

BALOZI OMBENI SEFUE ASTAAFU BILA YA KUPANGIWA KAZI NYINGINE

Aliyekuwa Katibu mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue sasa amestaafu bila kupangiwa kazi nyingine kama alivyoahidiwa na Rais John Magufuli siku aliyomteua Balozi Injinia John Kijazi kushika wadhifa huo na hivyo Balozi Sefue kutolewa kwa madai ya kupangiwa kazi nyingine.

Tarehe 6 mwezi Machi Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli alimteua John William Kijazi kushika wadhifa wa Katibu Mkuu kiongozi wadhifa ambao hapo kabla ulikuwa ukishikiliwa na Balozi Ombeni Sefue.Balozi Sefue alieteuliwa tena na Rais Magufuli Desemba 20, 2015 kuendelea kushika wadhifa huo kwa mkataba wa mwaka mmoja baada ya utumishi wake wa umma kuisha sambamba na makatibu wakuu na manaibu 50.

Katika uteuzi ule wapo makatibu wakuu na manaibu walioachwa akiwemo Dkt.Donald Mbando (Afya),Balozi Liberata Mulamula (Mambo ya Nje), Omari Chambo (Nishati na Madini), Jumanne Sagini(Tamisemi) na Joyce Mapunjo (Afrika ya Mashariki).Balozi Sefue alirudishwa tena lakini ghafla Machi 6 alisimamishwa na kumpisha Kijazi kwa maelezo kuwa atapangiwa kazi nyingine.

Lakini sasa imethibitika kuwa Balozi Sefue hatapangiwa kazi nyingine na kwamba muda wake wa kustaafu ulifika na hivyo hawezi kuendelea tena na utumishi wa umma.Akijibu maswali ya mwandishi wa gazeti la Mwananchi juu ya hatma ya makatibu wakuu na manaibu makatibu wakuu walioahidiwa kupangiwa kazi nyingine ,Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora) Dkt Laurean Ndumbaro alisema kuwa makatibu wakuu wote wamepata barua zao na hakuna ambae hana kazi isipokuwa kwa wale waliostaafu kwa mujibu wa sheria kama Balozi Sefue, Balozi Mulamula na Chambo ambao hana uhakika kama wanaweza kupangiwa majukumu mengine.

Swali ni je kama aliongezewa mwaka mmoja wa mkataba katika utumishi wa umma alipotolewa kwenye nafasi ile mara baada ya ueuzi kutenguliwa na Kijazi kuchukua nafasi yake mkataba wake ulivunjwa?Kama haukuvunjwa analipwa mshahara mpaka sasa kwa kazi gani anayoifanya?Kama ulivunjwa je Rais alimdanganya?

Chanzo: Tanzania Investiment Adventures
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top