Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KAULI ZA RAIS MAGUFULI ZAWA GUMZO NCHINI


Kauli mbalimbali zinazoendelea kutolewa na Rais John Magufuli, zimezua mjadala miongoni mwa wasomi nchini.

Kwa mfano, wanasema kauli ya kukosoa udahili wa wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) na ile ya kuelekeza hatua za kuchukua dhidi ya watu wanaotumia kimakosa barabara za Mabasi Yaendayo Haraka (Udart), inaashiria kuna tatizo kubwa la utendaji serikalini.

Walisema ni jambo lisiloingia akilini, wanafunzi wadahiliwe na kuanza masomo kisha baadaye wafukuzwe kwa maelezo kuwa Serikali haiwezi kulipia ada wanafunzi ‘vilaza’.

Akizungumzia kauli hizo jana, Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Dk James Jesse alisema hakuna sheria za usalama barabarani zinazotamka mtu akifanya kosa gari lake litolewe magurudumu.

Juzi wakati akiweka jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa maktaba ya kisasa ya UDSM, Rais Magufuli alisema mpango maalumu uliopitishwa na Serikali ya Awamu ya Nne wa wanafunzi kusoma diploma ya ualimu Udom, unajumuisha waliofeli.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria (OUT), Hamad Salim alihoji: “Rais amesema wanafunzi waliopo Udom ni vilaza ila waziri wa elimu (Profesa Joyce Ndalichako) alisema wanafunzi wanaosoma mafunzo hayo hakuna aliyepata daraja la nne. Sasa hapo nani mkweli.”

“Kupishana huku kwa kauli kunatupa mashaka na utendaji kazi wa baadhi ya viongozi serikalini."

Hamad alisema suala kama hilo lilipaswa kutolewa ufafanuzi na waziri husika na si Rais.

Alisema umefikia wakati wa kiongozi huyo mkuu wa nchi kubaini changamoto na kutoa maelekezo na si kuzungumzia kila kitu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top