Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SERIKALI YAONYA VIKALI MABENKI NA MAKAMPUNI YA SIMU KUONGEZA TOZO KWA WATEJA WAKE

Serikali imezuia Benki kupandisha viwango vya tozo katika miamala yake na kuelekeza gharama hizo kwa wateja wao. 

Kamishna Mkuu wa TRA, Alphayo Kidata amesema kuwa asilimia 18 ya VAT mpya iliyopitishwa kwenye miamala ya benki inahusisha gharama zilizokuwa zikitozwa na benki hizo kwa wateja wao lakini serikali ilikuwa haipati chochote.

Kidata amesema kuwa Benki Kuu imeelekezwa kudhibiti benki hizo kwa kufanya ujanja wa kuongeza makato kwenye miamala ya wateja wao wakati wakijua fika kuwa hilo si lengo la kodi hiyo mpya.

Ameelekeza kuwa kiwango cha kodi kinachotozwa kwenye miamala hiyo kinatakiwa kubaki kama mwanzo lakini serikali itakata kodi yake ya asilimia 18 na kodi nyingine zilizopo kwa mujibu wa sheria
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top