Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Majambazi, mali za wizi na silaha nzito vyakamatwa na jeshi la Polisi

Kikosi maalum cha kupambana na ujambazi wa kutumia silaha cha Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kimefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 5 wa makosa ya ujambazi wa kutumia silaha katika maeneo mbalimbali.

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam Kamishna Saimoni Sirro wakati akitoa taarifa ya kukamatwa majambazi wa 5 na kukutwa na silaha aina ya shotgun, bastola 3 na risasi 49.

Katika tukio lingine Polisi mnamo tarehe 5.9.2016 majira ya saa 8 usiku maeneo ya Magomeni mtaa wa Makumbusho waliokota begi lililokuwa na bastola mbili, sambamba na hilo wamefanikiwa kukamata magari 4 ya wizi, hati za magari na watuhumiwa wawili wa uhalifu huo wamekamatwa.

Jeshi hilo limetoa wito kwa viongozi wa serikali za mitaa kupitia kamati za ulinzi wa mitaa kuimarisha ulinzi na kuwataka wamiliki wa nyumba za kupanga kuhakikisha wanaweka kipengele cha kuwepo na picha katika mikataba ya kupangisha nyumba zao kutokana na uwepo wa wimbi la uhalifu.

Wakati huo huo Kamanda Sirro amesema Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kipindi cha siku 11 wamefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi 882,570,000 ikiwa ni tozo za makosa ya usalama barabarani na makosa mengineyo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top