Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Prof. Lipumba atimua Wakurugenzi CUF


Kila kukicha mgogoro ndani ya Chama cha Wananchi (CUF) unazidi kuchukua sura mpya. Jana viongozi wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi wamekutana kujadili mgogoro wa CUF sababu ni moja ya vyama vinavyounda UKAWA.

Viongozi wa UKAWA jana wametangaza kuwa hawamtambui Prof. Lipumba kama mwenyekiti wa CUF na kuwa wao watashirikiana na viongozi halali wa CUF, na kutilia maanani maazimio yaliy0pitishwa katika vikao halali vya CUF.

 Aidha, mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amewataka viongozi wa chama hicho nchini kote kumpuuza na kutompa ushirikiano Prof. Lipumba kwani ni msaliti.

Kwa upande wake yeye, Prof. Lipumba ameendelea kutekekelza majukumu yake kama Mwenyekiti wa CUF ambapo jana ametangaza kutengua uteuzi wa Wakurugenzi na Manaibu Wakurugenzi wa Idara mbalimbali za Chama cha Wananchi (CUF).

Wakurugenzi na Manaibu Wakurugenzi ambao uteuzi wao umetenguliwa ni pamoja na;-
  1.  Joran Bashange – Mkurugenzi wa Uchumi na Fedha
  2.  Ismail Jussa- Mkurugenzi wa Mambo ya Nje
  3.  Mustafa Wandwi- Mkurugenzi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama
  4.  Kurufumu Mchuchuli- Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Sheria
  5.  Shaweji Mketo- Naibu Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi na
  6.   Abdalla Mtolea- Naibu Mkurugenzi wa Mambo ya Nje
Aidha Prof. Lipumba amesema kuwa hajali kama viongozi wa UKAWA wanamtaka au hawamtaki kwani yeye anachojali ni kuijenga CUF.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top