Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RC Gambo awatumbua jipu watumishi watatu Halmashauri wilaya ya Ngorongoro

 Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo akitangaza kuwasimamisha kazi watumishi watatu wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro kwa tuhuma za ubadhilifu wa fedha za uchaguzi wa mwaka 2015.

Watumishi hao ni pamoja na Bi. Hadija Mkumbwa ambae alikuwa msimamizi wa uchaguzi wa mwaka 2015 na kumfuta cheo hicho,bwana Evansi Mwalukasa alikuwa mwekahazina wa halmashauri na  bwana Sembeli Sinayo yeye alikuwa mwanasheria wa halmashauri.

Maamuzi hayo yamefikia baada yakubainika kuna upotevu  wa fedha za uchaguzi takribani Milioni 188 ambazo matumizi yake hayakuwekwa  wazi na pia Milioni 20 zilitumika kwa manunuzi ambayo hayakufuata taratibu za manunuzi ya serikali.

“Kuanzi sasa nawasimamisha  kazi hawa watumishi watatu kwasababu wameisababishia serikali hasara ya takribani Milioni 128 ambazo zilikuwa fedha za uchaguzi”.

Aidha Mhe. Gambo alisema maamuzi hayo yametokana na taarifa aliyokabidhiwa na kamati aliyoiunda ya kuchunguza mapato na matumizi ya fedha za halmashauri hiyo na kubaini upotevu huo wa fedha nyingi ambazo amesema zingeweza kusaidia shughuli mbalimbali za uchaguzi katika Wilaya hiyo.

Amsema  fedha nyingine zimetumika kwenye manunuzi ambayo hayakufuata taratibu na sheria za manunuzi ya serikali  kinyume kabisa na taratibu za serikali katika maswala ya manunuzi.

Mhe. Gambo pia kasisitiza  watumishi wa serikali kufuata taratibu, sheria na kanuni mbalimbali katika kutekeleza majukumu yao ili kuepuka migongano na uvunjifu wa sheria mahala pa kazi na kupelekea kupoteza ajira  zao.
Watumishi wa Halmashauri ya Ngorongoro, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo (hayupo pichani) alipokuwa akitoa taarifa ya kamati ya uchunguzi aliyoiunda kuchunguza mapato na matumizi katika halmashauri hiyo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top