Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Rais Magufuli alivyoenda kumjulia hali Mkuu wa Mkoa Tanga Shigela aliyelazwa Muhimbili

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John PombeMagufuli, jana tarehe 19 Novemba, 2016 amemtembelea na kumjulia hali Mkuu wa Mkoa wa Tanga Bw. Martin Shigella ambaye amelazwa katika wodi ya Sewahaji iliyopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.

Bw. Martin Shigella alifikishwa hospitalini hapo tangu Jumatano iliyopita kwa ajili ya kupata matibabu.

Akimpa pole wodini humo Rais Magufuli alisema “Nakupa pole sana Ndg. Martin Shigella kwa maradhi yaliyokupata, nakuombea kwa Mwenyezi Mungu upone haraka na urejee katika kituo chako cha kazi ili uendelee na majukumu ya ujenzi wa Taifa”

Hali ya Bw. Martin Shigella inaendelea vizuri.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top