Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TUCTA yabariki uhakiki vyeti sekta binafsi

SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) limeunga mkono utaratibu wa serikali wa kuhakiki vyeti vya watumishi wa umma na kutaka utaratibu huo ufanyike pia kwenye sekta binafsi kama alivyoshauri Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Kikuu cha Iringa (Uol), Askofu Dk Owdenburg Mdegella.

Pamoja na shirikisho hilo, pia baadhi ya vyama vya wafanyakazi navyo vimeunga mkono utaratibu huo na kuitaka serikali ihakikishe inaondoa watumishi wote wanaotumia vyeti feki ili kutoa nafasi kwa wasomi wengi wanaohangaika mtaani kwa kukosa ajira.

Akizungumza na gazeti hili jana, Katibu Mkuu wa shirikisho hilo, Nicholaus Mgaya alisema uhakiki huo utasaidia kuondoa watumishi wengi wasiowajibika kwa kukosa sifa na kuhakikisha wale wenye sifa ndio wanapata ajira.

“Tunaomba huu uwe utaratibu wa nchi nzima, maeneo yote yaguswe na uhakiki huu kwa sababu ukweli uko wazi kwa sasa kuna watanzania wengi tena wasomi wa hali ya juu hawana ajira lakini nafasi zao zimezibwa na watu wasi na sifa,” alisisitiza Mgaya.

Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Sekta ya Huduma za Mtandao na Mawasiliano Tanzania (Tewuta), Yunus Ndaro alisema vyama vya wafanyakazi vinaunga mkono hatua hiyo ya serikali kwani itasaidia kurejesha heshima ya ajira nchini.

Alisema sekta binafsi pia ni sehemu ya Tanzania na inajiendesha pia kwa kufuata Sheria ya Ajira na Mahusiano ya Mwaka 2004, hivyo nayo inapaswa kuhakikiwa ili kuhakikisha inafuata misingi, kanuni na sheria za nchi.

“Mfano zipo kampuni nyingi za simu baadhi yake zikiwa binafsi zinaingiza wafanyakazi wageni kutoka nje ya nchi, wengi wakiwa hawana sifa, kupitia uhakiki huu haya yote yatavumbuliwa,” alisisitiza Ndaro.

Hata hivyo, alisema endapo serikali isipochukua uamuzi wa kuhakiki na sekta binafsi wale watumishi wa umma wote wadanganyifu watakaobainika kuwa na vyeti feki watakimbilia sekta binafsi hali itakayoendeleza zaidi tatizo la ajira.

Kwa upande wake, Mwanasheria wa Kujitegemea, Emmanuel Makene alisema uhakiki wa vyeti hivyo, unafanyika kwa mujibu wa sheria kutokana na ukweli kuwa sheria ya ajira inakataza mfanyakazi kughushi cheti.

“Hapa hakuna mtu wa kulaumiwa, serikali inatekeleza sheria kama inavyotaka, kifungu cha 338 na 342 cha Sheria ya Ajina na Mahusiano kiko wazi ni kosa la jinai kughushi. Na ni kweli watu wanaofanya hivi wapo lazima watafutwe na kuchukuliwa hatua,” alisisitiza Makene.

Wakati serikali ikiendelea na uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa serikali, hivi karibuni Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Kikuu cha Iringa (UOI), Askofu Dk Owdenburg Mdegella pamoja na kuipongeza serikali kwa kuanzisha utaratibu huo, pia ameomba ufanyike hadi sekta binafsi ili kupunguza ongezeko la vyeti bandia.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top