Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Bei ya maegesho ya magari yalalamikiwa


WADAU wa maegesho jijini Dar es Salaam, wameilalamikia mamlaka ya Jiji kwa kupandisha bei ya maegesho.

Bei hiyo imepanda kutoka Sh. 300 hadi 500 eneo la Posta na Sh. 100 hadi 500 eneo la Kariakoo.

Wakizungumza na Nipashe kwa nyakati tofauti, wadau hao walisema mtumiaji wa huduma hiyo amekosa mtetezi kwa kuwa mamlaka zinapandisha bei hiyo bila kuwashirikisha na hawana pa kuhoji.

“Kwa sasa ukiegesha gari kwa saa moja unalipa Sh. 500, kila siku naegesha gari, sijasikia matangazo ya kutujulisha mabadiliko ya bei hizo zaidi unakuta vijana wakusanya ushuru na ukibishana nao wanaita gari la kufunga gari lako na kwenda kulihifadhi hadi ulipe faini,” alisema Mohamed Juma, mkazi wa Mbezi ambaye huegesha gari lake eneo la Posta.

Source: Nipashe
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top