Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Uwoya apasua jipu la kumchukia Wema

Baada ya gazeti la Ijumaa kutoka na stori “Uwoya: Simpendi Wema” katika ukurasa wake wa mbele, muigizaji wa filamu Irene Uwoya amekanusha madai hayo kupitia ukurasa wake wa instagram.

Pia muigizaji huyo amedai yeye hana tatizo na Wema na sio mtu wa kuwekeana chuki na msanii mwenzake.

Kupitia instagram, Irene aliposti kipande cha gazeti hapo juu na kuandika

“Jamaniii sijawah sema simpend wema… Sina sababu ya kumchukia mim na mpenda kila Mtu na sinaga adui na wala sipend Kuwa na maadui na penda sana kuishi na watu vizuri… Hivo Ndivo nilivyo.”

Pia muigizaji huyo amedai wakati mwingine bifu huanzisha na waandishi wa habari pamoja na mashabiki.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top