Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Dk. Magufuli ataja mambo 10 atakayoanza nayo CCM

Leo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt John Pombe Magufuli ameongoza Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) kilichofanyika katika ukumbi wa Ikulu jijini Dar es Salaam.

Kikao hiki kilikuwa ni kikao chake cha kwanza tangu alipokabidhiwa mikoba ya kukiongoza cha hicho baada ya mwenyekiti aliyekuwepo Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kuomba kung’atuka kabla ya muda wake kuisha.

Akizungumza na wajumbe wa NEC leo, Dkt Magufuli ametaja mambo 10 ambayo anaanza nayo kama mwenyekiti wa CCM. Mambo hayo na haya yafuatayo;-
 
1. Rushwa
Mwenyekiti wa CCM Dkt Magufuli alisema kuwa chama hicho ni miongoni mwa taasisi zinazotuhumiwa sana kwa uwepo wa mianya ya rushwa hasa kipindi cha uchaguzi ndani ya chama au serikali. Amesema katika kipindi chake cha uongozi atahakikisha hakuna kiongozi atakayechaguliwa kwa kutoa rushwa.
 
2. Uimarishaji wa chama
Jambo la pili alilosema wakati akizungumza na wajumbe wa NEC zaidi ya 370 alisema kuwa ni kujenga chama imara kitakachoweza kuwatetea wananchi na kulinda rasilimali zao. Dkt Magufuli alisema wao wamechaguliwa na wananchi kupitia chama hivyo hawapaswi kuwa sehemu ya walalamikaji.
 
3. Wanachama
Chama ni wanachama, ndivyo alivyosema akielezea kuwa ni lazima chama kihakikishe kinaongeza udadi ya wanachama wake hasa vijana. Aidha, ametahadharisha kuwa wanachama hao wasiwe wananchama hewa, bali wawe ni wanachama wakukitumikia chama na watakaolipa ada.
 
4. Chama kujitegemea kiuchumi
CCM ina vitega uchumi vingi sana, lakini kila mara tunakuwa ni ombaomba hasa kipindi cha uchaguzi. Katika kipindi changu cha uongozi hili sitaki kuliona. Ni lazima tuhakikishe mali za chama zinakinufaisha chama na tuweze kujitegemea bila kuwa tegemezi kwa mtu yeyote, alisema mwenyekiti Dkt Magufuli.
 
5. Wasaliti na makundi
Kumekuwepo wanachama ambao si waaminifu ndani ya chama, hawa ni hatari ni lazima tuhakikishe tunakuwa na wanachama wakweli. Pia akizungumzia suala la makundi Dkt Magufuli alisema kuwa makundi ndani ya chama hasa wakati wa uchaguzi yamezidi kushamiri, na wengi huendeleza makundi hata baada ya uchaguzi, ni wakati wa kujenga CCM mmoja.
 
6. Chama Imara kuanzia chini
Hapa alieleza kuwa chama imara ni kile chenye mizizi kuanzia ngazi za chini. Ni lazima tuwe na chama imara kuanzia ngazi za shina, tawi, kata, wilaya, mkoa hadi taifa. Hili litafanukiwa kwa sisi tulipo huku juu kushuka hadi chini katika jitihada za kueleza sera zetu kwa wananchi.
 
7. Nafasi za uongozi
Mwenyekiti wa CCM amesema kuwa wakati wa mtu kuvaa kofia nyingi ndani ya chama ufike mwisho na kuwa sasa ni wakati wa nafasi moja ya uongozi kushikwa na mtu mmoja. Akifafanua hili alisema kuwa litasaidia kutoa nafasi kwa watu wengine pia kukitumikia chama.
 
8. Kufutwa vyeo
Akielezea katiba ya CCM, Dkt Magufuli alisema kuwa katika awamu yake ya uongozi anataka vyeo ambavyo havujatajwa kwenye katiba ya chama visiwepo. Akitoa mfano wa vyeo hivyo alisema ni pamoja na Jumuita ya Wazazi, Chipukizi.
 
9. Uwajibikaji
Alisema kuwa chama kina wajibu wa kuwatumikia wanachama wote bila ubaguzi. Alisisitiza kuwa katika awamu yake ya uongozi hatokubali kuona watu wachache wa vyeo vya juu wananufaika na chama na mamia ya wanachama wa chini wakiteseka.
 
10.  Nguvu ya chama
Jambo hili ambalo alilisema kwa msisitizo na hata kulirudia mara mbilia ni kuwa, anataka chama kinachoongoza wananchama na si wananchama au mwananchama anyeongoza chama. Akitilia mkazo hapa alisema mwanachama ndiye anapaswa kukifuata chama na si chama kumfuata mwanachama au wanachama wachache
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top