Loading...
'Scorpion' mtoboa macho akumbwa na balaa jipya
Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) amemuongezea shtaka la Kujeruhi mshtakiwa Salum Njwete maarufu kama Scorpion na sasa atakuwa na mashtaka mawili pamoja na lile la awali la unyang'anyi wa kutumia silaha.
Scorpion aliongezewa shtaka hilo na Wakili wa Serikali Nassoro Katuga, kabla ya kumsomea Maelezo ya Awali (PH).
Baada ya kusomewa maelezo ya awali, Scorpion alikubali hoja mbili na sita kuzikana.
Kutokana na maelezo hayo, hakimu mkazi wa mahakama hiyo, Flora Haule aliahirisha kesi hiyo hadi Desemba 14, mwaka huu kesi hiyo itakapoanza kusikilizwa.
Mshtakiwa amerudishwa rumande kutokana na moja ya shtaka linalomkabili kutokuwa na dhamana.
Post a Comment